Ticker

6/recent/ticker-posts

Waandishi Wa Habari Wanawake,Waripoti Michezo Kuongeza Wingi Wao Kwenye Vyombo Vya Habari.

 



Na Najjat Omar:

Mei 30,2024 Wizara Ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kupitia Waziri Wa Habari, Vijana, Utamaduni Na Michezo Tabia Maulid Mwita amewasilisha  Makadirio Ya Mapato Na Matumizi Ya Fedha Kwa Mwaka 2024/2025 amesema kuwa mwaka 2023/2024 jumla ya vyombo vya Habari za ra 45 vimekaguliwa Unguja na Pemba ni 14.

Katika hotuba yake Waziri Tabia amesema Zanzibar imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa mashindano makubwa ya mpira wa miguu Afrika yanayoitwa CAF African Schools Football Championship. Ni mashindano yaliyozikutanisha timu 14 (timu saba za Wanaume na timu saba za Wanaweke) za vijana wenye umri wa chini wa miaka 15 kutoka mataifa mbali mbali Afrika.

Kwa upande wa Tanzania bara kupitia kwenye Bajeti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeeleza hadi kufikia mwaka 2024 imesajili vituo vya Runinga 133, Redio 446, kebo 117 huku magazeti yakiwa 672.

Kuwepo wa takwimu hizo ni dhahiri kwamba ukuwaji wa tasnia ya Habari  kwa sasa inakuwa kwa kasi kubwa licha ya wingi wa vyombo vya habari ni sawa na kuwepo kwa vingi waaandishi wa Habari pia.

Licha hivyo utafiti uliofanyika mwaka 2019 na Baraza la Habari Tanzania – MCT unaonesha waandishi wa Habari Wanawake wengi wanaandika na kuripoti Habari za afya ,kilimo na jinsia.

Salma Abdul ni Mhariri Mkuu wa Radio ya Uyui Fm iliyopo Mkoani Tabora licha ya kuwa mhariri Salma pia ni muamuzi wa mchezo wa mpira wa miguu na mwandishi wa Habari za michezo amesema waandishi wanawake hawapendi kuandika na kuripoti michezo kwa sababu kwa upande wa michezo sio tu kujua kuandika bali pia ni kufahamu Elimu ya kina ya michezo.” Mimi nilipomaliza chuo nilianza kuandika michezo na nilipata mafunzo kutoka TFF ya uamuzi hivyo najua kanuni,sheria na hata miongozi ya mpira” Ameendelea kusema kwamba kwa sasa uandishi wa michezo sio kuandika tu bali ni kuchambua zaidi kwa kina.

Hali hii iko tofauti kwa Florencia Peter Meneja wa Vipindi kutoka Jembe Fm, radio iliyopo Mkoani Mwanza anayeongoza wafanyakazi 32 kati ya hao waandishi wa michezo ni watatu, wawili wanaume na mmoja ni mwanamke.”Waandishi wanawake wanaona kwamba kuwa mwaandishi wa michezo ni kazi ngumu na ni sehemu ya wanaume jambo ambalo halina ukweli” Florencia anasema walipoanza kupata mtangazaji wa kike kwenye vipindi vya michezo wameongeza wasikilizaji.

Ripoti ya mwaka 2023 ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania -

TCU imeonesha kuwa wanafunzi 261,555 wamehitimu vyuo vikuu kati ya mwaka 2018 hadi 2022 huku kati hao waliosomea Uandishi wa Mawasiliano ya Umma ni 3,634.

Flora Mwakasala ni Mhariri wa Kilimanjaro Revival Fm redio iliyopo Mkoani Kilimanjaro akiwa kiongozi ambaye anasimamia wafanyakazi 13 amesema si kwa wafanyakazi tu bali hata jamii inaona kwamba mwandishi mwanamke kuwa kwenye michezo ni suala ambalo haliko sahihi “Kuna dhana kwamba Habari za michezo ni wanaume tu sio Wanawake wanaweza kuandika hio ndio naona ni sababu ambayo kunakuwa na uhaba wa waandishi Wanawake kwenye upande wa michezo” Ameshauri kuwa ni vyema waandishi wajue na wajifunze juu ya Elimu na masuala ya michezo licha ya kuwa wanahabari.

Ziada Kilobo ni Msimamizi wa Uendelevu wa Taasis katika Baraza la Habari Tanzania – MCT amesema kwa miaka sita sasa Baraza la Habari Tanzania limekuwa likitekeleza mradi wa kuwawezesha waandishi wa Habari ambao ni viongozi waliopo kwenye vyumba vya Habari pia kuna utaratibu maalum unaowalea waandishi wa Habari wachanga ambao wanajikita katika masuala ya kimichezo.”Kwanza ni fursa kwa mwaandishi mwanamke ambaye amejikita kwenye uandishi ,kwa sababu si wengi waliojikita huko, kwa kudhani kuwa huko hakuna fursa ila ni ukweli kwamba kwenye uandishi wa michezo kuna uhaba mkubwa wa waandishi wanawake na hilo tumeliona na tunalifanyia kazi kwa kuwahamasisha zaidi” Amemaliza Ziada.

Utafiti uliofanywa na Taasis ya Wanawake wa Afrika kwenye michezo unaonesha waandishi wa Habari waliopo kwenye vyombo vya Habari wengi wao wamesomea taalum nyengine na kisha kusomea uamuzi ndipo wanapopata nafasi ya kuwa waandishi na wachambuzi.

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake – TAMWA -Z kinatekeleza mradi wa mwaka mmoja ambapo umewapatia mafunzo waandishi wa Habari 20 Kutoka Unguja na 10 kutoka Pemba kuleta ushawishi wa kuandika na kuripoti  ujumuishaji wa michezo wa wasichana na Wanawake kwenye sekta ya michezo.

Post a Comment

0 Comments