Ticker

6/recent/ticker-posts

Pondeza Aahidi Kutatua Changamoto Za Wanafunzi Wanawake Chumbuni


Mbunge Wa wananchi wa Jimbo la Chumbuni  Ussi Salum Pondeza  amekutana na wanafunzi  wanawake  Wa Madrasa  mbalimbali  za jimbo la Chumbuni kwa lengo la kutatua Changamoto zao Zikiwemo Vikalio, Mafeni, Ukarabati Wa Nadrasa.

Katika mazungumzo yao Pondeza alisema yale yote yaliyo katika uwezo wake atayafanikisha ili utoaji na upatikanaji wa elimu uwe katika mazingira bora.

“Nitahakikisha nafanikisha yale yote yaliyo katika uwezo wangu kwa haraka” Alisema

Aidha mbunge huyo aliwasisitiza wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili kuona jimbo hilo linakuwa ba wataalamu wengi wa masomo ya dini ya kiislamu.

“Jimbo hili linategemea uwepo wa wataalamu wa masomo ya dini ya Kiuslamu hivyo someni kwa bidii kufikia lengo hilo” Aliongezea

Wanafunzi hao walimuahidi mbunge huyo kusoma kwa bidii ili kufanikisha lengo la kuwepo kwa wataalamu hao.

Post a Comment

0 Comments