Ticker

6/recent/ticker-posts

Ulemavu Usiwe Kwikwazo Cha Kutosoma: Abeida Rashid

 

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Abeida Rashid Abdallah akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa vyoo rafiki vya watoto wake wenye ulemavu, iliyoandaliwa na Taasisi ya Maisha ya Amani kwa Watoto wenye Ulemavu, hafla hiyo imefafinya leo katika viwanja vya Skuli ya Sekondari ya Jangwani, Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Abeida Rashid Abdallah amewataka Watoto wakike wenye ulemavu kutoona hali hiyo kwamba ni kikwazo cha kutosoma  na kukatisha  ndoto zao za Maisha.

Akizungumza na wasichana hao katika uzinduzi wa vyoo rafiki kwa Watoto wa kike wenye ulemavu uliyofanyika katika skuli ya Sekondari ya Jangwani Dar Es Salaam, hafla hiyo imeandaliwa na Taasisi ya Maisha ya Amani kwa watu wenye ulemavu, amesema anaelewa changamoto zinazowakabili wasichana hao lakini hawatakiwi kukataa tamaa katika kutafuta elimu ili wawe viongozi wa baadae.

Amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinazungumza masuala ya watu wenye ulemavu kwenye vyombo vya maamuzi ili kuhakikisha watu wenye ulemavu hawajaachwa nyuma.

Amesema nchi ya Tanzania inamingozo mbali mbali ambayo inasimamia masuala ya watu wenye ulemavu ikiwemo UN Covection on the right of People with disability pia kunasheria  ya Tanzania Bara ya 2010 kwa upande wa Zanzibar kuna sheria namba  9 ya mwaka 2006 ambayo imefanyiwa marekebisho mwaka jana, sheria zote hizo zinazungumzia wajibu wa utambuzi wa haki kwa watu wenye ulemavu, usawa na kutokubaguliwa, kukuza uelewa, n.k.

Aidha Katibu Mkuu huyo ametoa wito kwa walimu wote katika skuli mbali mbali kuweka vyoo rafiki kwa Watoto wenye ulemavu, na sio vyoo tuu hata njia ili mazingira nayo yawe rafiki ili wajihisi wako na amani.



Naye Mkurugezi  wa Taasisi ya Maisha ya Amani kwa watu wenye ulemavu, Sofia Mbeyela amesema mradi huyo wa ujenzi wa vyoo rafiki kwa Watoto wa kike wenye ulemavu umeanza Julai mwaka jana na umegharibu milioni 20,000 kwa kujenga vyoo vine na chumba kimoja kwaajili ya wasichana hao kubadili nguo wakati wakiwa katika siku zao za hedhi.

Aidha amewashukuru wadau wote waliyojitokeza kwa hali na mali katika kuchangia ujenzi huo  kwani hapo awali skuli hiyo ilikuwa na vyoo rafiki vitatu huku wanafunzi wakiwa 110.

Amesema mradi huo utaendelea kwa skuli zote hivyo amewaomba wananchi, viongozi, mashirika/taasisi za umma na Serikali kuendelea kuchangia mradi huo ili kuwaondolea Watoto wenye ulemavu changamoto hiyo.

Kwa upande wa wanafunzi wenye ulemavu, akizungumza Zulfa Swaleh mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Skuli ya Jangwani amesema amefarajika na ujenzi wa vyoo lakini pia amewaomba wananchi kujitokeza kuwasaidia madaftari na vitavu kwani wengi wao ni Watoto wa familia za kipato cha chini.

 

Mkurugezi  wa Taasisi ya Maisha ya Amani kwa watu wenye ulemavu, Sofia Mbeyela  na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Abeida Rashid Abdallah ni watu mweney ulemavu hivyo wanaelewa changamoto zinazowakabili Watoto wenye ulemavu na wataendelea kupambana ili kuhakikisha watu wenye ulemavu hawajaachwa nyuma.

Post a Comment

0 Comments