Ikiwa msimu wa 2022-23 umemalizika na Azam FC
kutoambulia chochote ndani ya msimu mzima sasa klabu hiyo imeanza na uboreshaji
wa kikosi chao kuanzia kwa wachezaji na Benchi la ufundi.
Katika maboresho hayo ni kuanza kuondoa wale ambao
hawana mahitaji nao katika msimu ujao ambapo leo wameanza na kuondoa viongozi
wawili wa benchi la ufundi pamoja na wachezaji watatu.
Waliachwa kwenye benchi la ufundi ni Kocha wa
Magolikipa raia wa Uhispania Daniel
Caden na Kocha wa Viungo Dkt. Moadh Hiraou huku taarifa ya klabu
hiyo ikieleza ni makubaliano ya pande zote mbili.
Upaande wa wachezaji
waliochwa ni pamoja na beki kisiki Bruce Kangwa aliyehudumu klabuni hapo kwa
miaka saba ya nguvu, tokea aliposajiliwa mwaka 2016 ukitoka Highlanders FC ya
Zimbabwe.
Wachezaji wengine
waliopewa mkono wa kwaheri ni mshambuliaji Rodgers Kola raia wa Zambia, na
kiungo Kenneth Muguna raia wa Kenya.
Ikumbukwe ni karibia
wiki moja tangu klabu hiyo imtambulishe kiungo mzanzibar Feisal Salum Abdalla
aliyetokea Yanga ambaye atahudumu klabuni hapo kwa mkataba wa miaka mitatu.
0 Comments