Ticker

6/recent/ticker-posts

Waandishi Wa Habari Wasema Mamlaka Ya Baadhi Ya Taasisi Ni Kubwa Dhidi Ya Vyombo Vya Habari



 
Picha Kwa Msaada wa DW

NA Ahmed Abdulla:

Licha ya sauti zinazopazwa na wadau mbalimbali ikiwemo chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa-Zanzibar pamoja na Internews kuhusu uwepo wa uhuru wa kujieleza kwa makundi mbalimbali lakini bado makundi mengi kiuhalisia yananyimwa uhuru wa kujieleza na makundi minginekutokana na mfumo wa sheria kuyapa nguvu makundi hayo.

Miongoni mwa kundi lisilo na uhuru wa kujieleza mbele ya wengine ni waandishi wa habari ambapo mifano mingi inaonyesha waandishi wa habari kunyimwa uhuru katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mfano mdogo tu ni ule wa mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi Jessy Mikofu kupata manyanyaso kutoka vikosi vya SMZ vilipokuwa vikifanya majukumu yao ya kuwatawanya wafanyabiasha wadogo wadogo waliokuwa hawapo kisheria.

Huo ni mfano unaoonyesha waandishi kunyimwa uhuru wa kutekeleza majukumu yao hali inayoleta hofu kwa waandishi kuibua mambo mazito kwa maslahi ya taifa.

Hilo lilikuwa ni jicho la Zanlight Blog lakini tulifunga safari kuwafata waandishi wenyewe jee wanasemaje kuhusu uhuru wao.

Omar Abdulla ni muandishi wa habari wa East Afrika TV kwa upande a Zanzibar yeye anasema uhuru uliokuwepo ni wa kusifia watu wa jamii Fulani tu lakini ukiamua kufatilia mapungufu yao unaanza kupokea vitisho hali inayowapunguza ari ya ufautiliji wa mambo mbalimbali.

“Thuru tulionao ni wa kusifia tu na si wa kukosoa tunapokosoa tunakuwa ni waja wa kupokea vitisho tu” alisema Omar

Amesema katika kutafuta mwarobaini wa hilo kuna kila sababu ya kuangalia upya nguvu zilizotolewa kwa baadhi ya makundi na uhuru wa waandishi wa habar.

“Tunahitaji uhuru wetu ulioainishwa kwenye sheria uheshimiwe na makundi yote na wao pia wapunguziwe nguvu walizopewa” aliongezea

Dhulkaada Khamis kutoka Zenj Online TV ameseama ndio kwanza anaingia kwenye tasnia ya habari lakini ana hofu ya kuandika habari za uchunguzi kwani hao waliomtangulia nao pia anahisi wanahofu.

Amesema ili kuisaidia serikali katika kuibua mambo mbalimbali basi waandishi wanatakiwa kuwa na uhuru wa kweli kwani kwa sasa uhuru wao ni kama umezuiwa na makundi mingine.

“Tunaambiwa tuna uhuru lakini ninavyoona uhuru wetu umeporwa tuachiwe tisaidie serikali yetu” alisema Dhulkaada

Kwa upande wake Kher Abdulqadir Kheir ambaye ni muandishi wa habari wa kujitegemea amesema kwa miaka mitano iliyopo uhuru wa vyombo vya habari ulianza kupotea japo wanapambana kuona wanapata sheria bora zitakazowapatia uhuru wa kweli.

 

Aidha amesema kwa muandishi mwenyewe ndio uhuru umekosekana kabisa kwani hata anapoandaa habari yenye kuonyesha madhaifu ya watu wa tabaka fulani basi kuna uwezekano wa habari hiyo isitolewe na Mhariri wa chombo cha habari kwa horu ya kufungiwa chombo cha habari hicho.

 

"Kwa muandishi wa habari ndio kwenye tatizo zaidi kwana anaweza kuandaa habari yake lakini mhariri akaikataa kwa kuhofia kufungiwa chombo chao cha habari" Amesema Kher  Abdulqadir

Kulingana na waliyoyazungumza waandishi wa habari na mfano tulioutoa hapo juu basi kuna sababu kwa Serikali kuweka sheria itakayotoa uhuru wa kweli kwa waandishi wa habari na vyombo vya habari ili kuona sekta hiyo inaisadia serikali kuibua changamoto katika sekta mbalimbali za umma kwa lengo la kufikia maendeleo ya kweli.

 


Post a Comment

0 Comments