Ticker

6/recent/ticker-posts

JEE MALINDI KUENDELEZA UBABE WAKE LIGI KUU ZANZIBAR?

 

Ligi kuu ya Zanzibar ZPL itaendelea leo Disemba 11 kwa michezo mitatu katika viwanja tofauti kisiwani Unguja.

Mchezo wa kwanza utachezwa katika kiwanja cha Amani majira ya saa 10:00 za alaasiri kwa timu ya black sailor watakapoikaribisha timu ya police

Katika mchezo uliyopita ikiwa ni wa mzunguko watatu timu ya Black Sailor ambayo ipo nafasi ya 5 ikiwa na alama zake 4 ikiwa imeshacheza jumla  michezo mitatu ilipoteza kwa kufungwa mabao 3-1 dhidi ya timu ya Malindi huku timu ya Police ambayo inashikilia mkia ikiwa nafasi ya 12 ikiwa na alama yake 1 ikiwa imecheza michezo yake mitatu ilikwenda sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya timu ya Zimamoto.

Mchezo mwengine ambao utapigwa leo hii ni mchezo kati ya timu Chuoni dhidi ya timu ya Mlandege ambao utapigwa majira ya saa 10:00 za alaasiri katika kiwanja cha Mao A.

Mchezo uliopita timu ya Chuoni ambayo ipo nafasi ya 10 ikiwa na alama yake 1 ikiwa imeshacheza michezo yake miwili ilitoa sare ya 0-0 dhidi ya timu ya timu ya Black Sailor ambapo timu Mlandege ambayo ipo nafasi ya 7 na alama zake 3 ikiwa imeshacheza michezo miwili ilipoteza mbele ya timu ya Kipanga kwa kufungwa bao 1-0.

Pia katika Dimba la Mao B kutakuwa na mchezo kati ya Malindi dhidi ya KVZ majira ya saa 10:00 za alaasiri, ambapo katika mchezo uliopita timu ya Malindi ambayo ndio vinara wa ligi kuu ikiwa na alama zake 9 kibindoni ikiwa imeshacheza michezo mitatu ilipata ushindi mnene wa mabao 3-1 dhidi ya timu ya Black Sailor huku timu ya KVZ ikiwa ipo nafasi ya 8 ikiwa na alama zake 3 na imeshacheza michezo miwili iliishinda kwa kuifunga timu ya Hard Rock mabao 3-2.


MSIMAMO WA LIGI KUU YA ZANZIBAR KWA SASA

Post a Comment

0 Comments