Na
Thuwaiba Habibu, Zanzibar:
Mara tu baada ya kushika usukani wa kuiongozi
Zanzibar karibu miaka mitano iliopita Rais Hussein Mwinyi alionyesha
ushirikiano mkubwa na vyombo vya habari
Matamshi na
hatua yake ya kuonana na waandishi mara kwa mara katika miaka mitatu ya kwanza
ya uongozi wake yalitoa sura ya kuimarika mashirikiano kati ya serikali na
wadau wa habari.
Msingi wa kuaminiana ukawekewa zege na
kilichosubiriwa ni ujenzi utaopelekea maelewano hayo kuwa mazuri zaidi siku
hadi siku.
Wakati huo waandishi na wadau wa habari wakawa na
matumaini makubwa ya kilio chao cha zaidi ya miaka 20 sasa cha kuwa na wigo
mpana wa uhuru wa habari, haki ya kujieleza na mazingiza bora ya kazi kwa wana
wa taaluma ya habari kimesikika.
Ndoto hii ilionekana karibu kutiumia Dk. Mwinyi
alipoagiza mara kwa mara kuchukuliwa
hatua za kisheria na utendaji kwa
taasisi za serikali na mashirika ya umma kuwa karibu na vyombo vya habari ili
umma upate taarifa sahihi za shuhuli za
serikali yao.
Katika msisitizo wake alisema wataowakwepa waandishi au kukataa kutoa
ufafanuzi juu ya masuala mbali mbali hawafai kuwemo katika serikali yake.
Lakini kwa bahati mbaya kauli zote zile
zimeonekana kupotea hewani kama moshi huku waandishiwa habari wakiendelea
kuambiwa wavumilie na wakati wowote ule
wataona mabadiliko.
Hivi sasa bado Zanzibar yapo malalmiko na
masikitiko ya wanahabari kunyimwa taarifa juu ya masuala ambayo wananchi
wanataka wapatiwe maelezo au ufafanuzi.
Mwanahabari wa kujitegemea, Muhammed Khamis, anakumbusha haki ya kikatiba na kisheria kwa waandishi wa habari kupatiwa taarifa na hii imeainishwa
wazi wazi katika Katiba yaZanzibar ya
mwaka ( 1984) katika Ibara ya 18(1) na (2) inayoeleza kwamba Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu
yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta kupokea
nakutoa habari na dhana kupitia chombo chochote, bila ya kujali mipaka ya nchi,
na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
Vile vile imeelezwa kila raia anayo haki ya kupewa
taarifa wakati wote kuhusu matukio mbali mbali nchini na duniani kote ambayo ni
muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu
kwajamii.
Lakini
unapokwenda kwa muhusika wa kukupa taarifa anakakataa kutoa taarifa, alieleza.
Mara nyingi
udhibiti uliopo katika sheria ziliopo Zanzibar hivi sasa umeweka mazingira ya
wanaohusika na kutoa taarifa na wao kutoruhusiwa kuzungumzia masuala ya taasisi
zao.
Hapa ndipo kwenye utata, kama mtu anaambiwa anao
uhuru uliotamkwa ndani ya katiba wa kupata taarifa sasa inakuwaje kuwepo sheria na kanuni
zinazokiuka katiba za kuzuwia upatikanaji wa taarifa?
Mwandishi wa habari wa The Chanzo, Najjat Omar,
ambaye amekuwa akikutana na kadhia hiyo anasema kikwazo cha waandishi kukosa
taarifa ni utendaji usio mzuri wa baadhi ya maafisa wa serikali ambao hawataki
kutekeleza wajibu wao wa kujibu changamoto za wananchi ambazo wao ndio wahusika wa kuzishughulikia.
"Waandishi wanashindwa kufanya uwiano wa
habari wanazoziandika kutokana na kukosa taarifa kwa baadhi ya watumishi wa
serikalini. Hii inatokana na woga ama kwa kuweka vikwazo vya kupeleka maswali
au barua,"aliongeza.
Suala la kupeleka maswali kwa maadishi kama vile
mtu anajaza fomu ya maombi si la kawaida katika sekta ya habari katika nchi
ambazo zinaendesha shughuli zake kwa misingi ya kidemokrasia
Jambo jengine ambalo mfumo huu unapelekea umma
kukosa habari kwa wakati ni kwa sababu baadhi ya mambo huwa yanahitaji maelezo
ya haraka kwa vile usumbufu wake unaathiri maisha ya kila siku ya wananchi.
Mifano halisi ni kama ya kuwepo eneo la makazi ya
watu kujaa taka ambazo hazijakusanywa kwa muda mrefu na kuhatarisha maisha.
Lakini wakati huo huo maofisa wa Manispaa au
Halmashauri wanasumbua wananchi kwa kukusanya malipo ya usafi wa mazingira,
yaani fedha za usafi zinakusanywa lakini taka haziondolewi.
Hapo
mandishi anapokwenda kutaka maelezo anaambiwa apeleke kwa maandishi.
Mbona makusanyo ya malipo ya usafi wa mazingira hayapelekewi maombi kwa
wananchi kwa maandishi?
Kwa kweli mtindo huu wa kudai maandishi kwanza ni
sawa na kumwambia mwenye njaa andike
barua ya maombi ya kueleza ana njaa na anataka chakula. Kwa mwenendo huu, si
ajabu pakazuka masuala ya kumtaka mwenye njaa aseme aina gani ya chakula
anaomba.
Huu sio mwendo mzuri na pale panapokuwapo na sheria nzuri za habari
na haki ya kujieleza ndio usumbufu wa aina hii
unaohatarisha maisha ya watu ndio utaondoka au angalau kupungua.
Serikali ya Zanzibar inapswa kutambua waandishi wa
habari ni washirika muhiumu wa maendeleo na wanapodadisi lengo ni kuwahimiza
watumishi wa umma kufanya kazi kwa uwadilifu na wanaofanya uzembe kuwajibika.
Najjat ameiomba serikali iwekeze nguvu kwa maafisa wa habari waliopo katika wizara na
idarakwa na mamlaka ya kuwasaidia waandishi ambao hawako katika sekta ya habari
serikalini kupata majibu ya maswali ya
wabnayotaka wapatiwe ufafanuzi.
Hayo masuala huo ndio mwananchi wa kawaida huwa
anauliza na kwa kuwa haiwezekani kila mtu kwenda wizarani kupeleka masuala ndio
maana kazi hio hufanywa na waandishiwa habari kwa niaba ya umma.
Zulfa Juma
Silima mwandishi kutoka Tiffu Tv amesema
uhusiano kati ya serikali na
wanahabari hauridhishi na unapaswa
kuangaliwe ili pawepo mazingira mazuri ya kisheria ili mashirikiano yawe mazuri
kwa maslahi ya nchi.
Mara nyingi Serikali hukimbilia kuviita vyombo vya
habari ikitaka kupeleka ujumbe wa aina
moja au nyengine kwa jamii na hasa kufikisha taarifa muhimu.
Lakini wana habari wanapoona dosari maeneo fulani
wamekuwa wazito au kukataa kabisa kutoa ushirikiano na mara nyengine hata
kuweka vikwazo na visingizio huwa vingi. Hasa panapokuwepo masuala ya kisiasa,
usalama wa raiya na mali zao au panapotakiwa maelezo juu ya matumizi ya fedha
za umma.
"Kwa Zanzibarkupata baadhi ya taarifa inakuwa
ni rahisi na kwa matukio mengine inakuwa shida aliongeza.
Mwanaharakati na Mtetezi wa Masuala
ya Habari, Juma Khamis Juma,
anasema anavyoona ni muhimu kuwa uhusiano mzuri kati ya serikali na vyombo vya
habari na pasiwepo vikwazo katika kutoa taarifa.
Alisisitiza kwamba uwazi ni nguzo umuhimu katika
kuimarisha utawala bora na wa kidemokrasia.
Alisema pale ambapo hapana vikwazo inakuwa rahisi
kwa waandishi wa habari kuisaidia Serikali yao na jamii kuibua vitendo vyenye
harufu ya rushwa na ufisadi na umma kuwa na uelewa mzuri wa shughuli za
serikali zinavyoendesha.
Uwazi pia unasaidia kupunguza uvumi usiokuwa na
tija kwa nchi, aliongeza.
Amesema ni vizuri kuwa sheria mpya na rafiki za
vyombo vya habari ambazo zitaiyafanya uhusiano kati ya serikali na wanahabari
kuwa mzuri..
Hii itasaidia waandishi kutoa taarifa sahihi na
kwa wakati kwa umma na wakati huo Serikali kupokea maoni ya jamii ili mwisho wa
siku yasaidie kuiletea Zanzibar maendeleo.
Mwandishi
na mwalimu wa aTasnia ya habari ndani na nje Zanzibar ambaye naye amekuwa
mstari wa mbele kutaka mabadliko ya sheria za habari, Salim Said Salim, amesema
wigo mpana wa uhuru habari ni nyenzo nzuri ya kujenga utawala bora na
kuimarisha demokrasi katka nchi.
Amesema pale ambapo shughuli za serikali
zinaendeshwa kwa uwazi, kama alivyoahidi Dk. Mwinyi aliposhika nafasi ya
uongozi, imani ya wananchi kwa serikali yao huongezeka na hutoa mashirikiano
mazuri.
Amesema sheria za hivi sasa sio rafiki hata kidogo
kwani zinabana uhuru wa habari na kujieleza na hii haina maslahi mazuri kwa
Zanzibar.
Aliitaka Serikali kutimiza ahadi yake na kuangana
nchi kadha za Afrika zikiwemo jirani ambazo leo zinapigiwa mfano wa kuwa
nasheria nzuri za habari.
Aliitaka Serikali kutokuwa na hofu na kupanua
uhuuru wa vyombo vya habari kwani lengo la waandishi ni kutaka sheria
zitazowawezesha kufanya kazi zao kwa uweledi na kutetea maslahi ya watu wa
Zanzibar na sio kumkomoa mtu au kikundi cha watu.
Alisema Kenya, Rwanda, Namibi ,Ghana na hata
Uganda na Tanzania Bara zimefanya
mabadiliko ya sheria ambayo anagalau kama sio mapana sana, lakini sio yale
yanayowabana waandishii mbavu na koo.
Sasa ni
karibu miaka 20 tokea kilio cha kutaka sheria rafiki za habari na kila
panapotolewa ahadi ya mchakato kuwa mbioni au kufikia tamati ndio kitabu
hufungwa na kazi huanza upya ya alifu kwa kijiti.
Wiki chache ziliopita tulisikia kazi imemalizika
zaidi ya asilimia 80 na wakati wowote marekebisho ya sheria yatafikishwa Baraza
la Wawakilishi.
Ghafla upepo ulibadilika , kama ilivyo katika
bahari inayovizunguka visiwa vya Ungua na Pemba, kwa kuambiwa pole pole ndio
mwendo na kwahivyo waandishi na wadau wa habari wa subiri mwakani, mwaka ujao
au mine au mitano itayofuata na sio kabla ya kufanyika uchaguzi wa mwezi Oktoba
, mwaka huu.
Miaka 20 imepita na kila siku hali ni kama ile
nyimbo ya taarabu isemayo Kila siku
waniamnbia kesho, keshokwa nini ukweli hutaki nambia.
Ni vizuri kwa ziliotolewa kila kukicha
zikatelekezwa. Ahadi ni deni na Waarabu wansema “Laa takliful miaad, yaani
usiende kinyume na ahadi yako”.
Utawala bora huimarika panapokuwepo uwazi, uhuru
wa habari na haki ya kujieleza na papokosekana huwepo mashaka na kutoamini.
Ni miuhimu kwe sheria hii kupewa umuhimu kama
zilivyo sheria zinazohusu taaluma nyengine
0 Comments