Ticker

6/recent/ticker-posts

Sheria Mpya Ya Habari Zanzibar Bado Ni Kitendawili

 


NA SITI ALI,ZANZIBAR

WADAU wa vyombo vya habari wameiomba serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kukamilisha mchakato wa marekebisho ya sheria za habari zilizotolewa maoni na wadau ili  kutoa mazingira rafiki kwa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao bila vikwazo.

 Kwani ni muda mrefu sasa licha ya wadau mbalimbali kutoa na kuwasilisha mapendekezo yao kuhusu mapungufu yaliyopo kwenye baadhi ya sheria hizo, lakini utekelezaji wake bado umekuwa wa kusuasua jambo linalopelekea mazingira magumu ya utendaji kazi wa vyombo vya habari nchini.

Wadau wa habari wamefanya mapitio ya sheria nane za habari ikiwemo Sheria ya usajili wa wakala wa habari, magazeti na vitabu namba 5 ya mwaka 1988 iliyofanyiwa marekebisho na sheria no.8 ya 1997, Sheria ya Tume ya Utangazaji Zanzibar namba 7 ya mwaka 1997  iliyorekebishwa na sheria namba 1 ya mwaka 2010 na kuwasilisha ripoti ya mapendekezo yao kwa mamlaka husika ikiwemo kukutana na Rais na waziri.

Afisa program wa masuala ya utetezi na uchechemuzi kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA –ZNZ) Zaina Abdallah Mzee amesema kuwa wanachukuwa jitihada mbali mbali za kuzisemea sheria zote zinazohusu habari ambazo haziko huru na rafiki kwa waandishi wa habari na vyombo vya habari  ambazo ni sheria ya Wakala wa Habari Vitabu na Magazeti ya mwaka 1988,sheria ya Tume ya Utangazaji,sheria ya Uchaguzi na nyenginezo ambapo sheria zote hizi zinawakwaza waandishi wa habari na vyombo vya habari na badala yake kupendekeza kuwekwa sheria moja tu ambayo ni rafiki kwa waandishi wa habari na vyombo vya habari katika kazi zao.

“Tumekuwa tukipaza sauti zetu kwa muda mrefu sasa kupatikana sheria mpya ya habari Zanzibar kuzisemea sheria ambazo zinawakwaza na zina mapungufu kwa waandishi wa habari na badala yake kupendekeza sheria moja tu ambayo ni rafiki kwa waandishi wa habari”anaeleza Zaina.

Aidha Zaina ameelezea mashirikiano yao baina ya Jumuiya waandishi wa habari na maendeleo Zanzibar ( ZAMECO) na Serekali Ikiwa ni pamoja na kukutana na kufanya mazungumzo viongozi wa nchi akiwemo Rais na Waziri wa habari ,Tume ya kurekebisha sheria ,Idara ya habari maelezo, wajumbe wa baraza la wawakilishi ambapo wote hawa wamekiri kuwepo kwa mapungufu katika sheria ya habari iliyopo.

“Mashirikiano ni mazuri baina yetu na Serekali kwani tumepata kufanya mazungumzo na viongozi mbali mbali wa  nchi akiwemo Waziri wa habari,Tume ya Utangazaji,Tume ya kurekebisha sheria,Idara ya habari maelezo,wajumbe wa baraza la wawakilishi na kukiri kuwepo kwa mapungufu katika sheria ya habari iliyopo na kuwahidi kufanyia marekebisho na badala yake kupendekeza kuwepo kwa sheria moja tu itakayokidhi vigezo vya habari”ameeleza Zaina.

Hata hivyo ameelezea mikakati waliyojiwekea katika kupaza sauti juu ya mapungufu yaliyomo katika sheria iliyopo na kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari wachanga kuripoti masuala ya sheria yahabari iliyopo, kupigania kuwekwa kwa sheria mpya ya habari ambayo ni rafiki kwa waandishi wa habari sambamba na kutoa wito kwa Serikali na wadau wa habari(watunga sera)kufanya hima suala la sheria mpya ya habari kwani sheria iliyopo sio rafiki  kwa waandhishi wa habari na vyombo vya habari.

“ Wito kwa Serekali na wadau wa habari pamoja na watunga sera na sheria kufanya hima suala la sheria mpya ya habari kwani ni kilio kwa waandishi wa habari ambapo sharia iliyopo sio rafiki  kwa waandhishi wa habari na vyombo vya habari kwani kufanya hivyo kutapelekea kupata maendeleo katikakwani mwandishi wa habari ni sauti ya wasio na sauti “amesema Zaina.

Akifafanua kuhusu maendeleo ya mchakato wa mabadiliko ya sheria za habari Zanzibar, Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar ,Salum Ramadhan Abdallah alieleza kuwa sheria ya habari ipo tayari kufanyiwa marekebisho kwani tayari mapendekezo ya sheria hizo zipo katika hatua nzuri kwani imeanza kuchukuliwa maoni.

 Wadau mbali mbali,hivyo atahakikisha sheria hii ataisimamia hadi kupitishwa,kwani ni ya muda mrefu sasa tokea kutolewa maoni,  ulipoanza mchakato wa sharia mpya  ,hivyo ameahidi kufika mwisho wa suala hili hivi karibuni.na kuwatoa hofu wanahabari juu ya suala zima la kupata sharia mpya ya habari.

"Kwa sasa  sheria ya habari ipo tayari kufanyiwa marekebisho kufanyiwa marekebisho kwani tayari mapendekezo ya sheria hizo zipo katika hatua nzuri kwani imeanza kuchukuliwa maoni na wadau mbali mbali,hivyo nitahakikisha sheria hii kuisimamia hadi kupitishwa,kwani ni ya muda mrefu sasa tokea kutolewa maoni,hivyo ameahidi kulifikisha  mwisho suala hili la sheria mpya hivi karibuni,

Nawatoa hofu wanahabari juu ya suala zima la kupata sheria mpya ya habari ambayo itakwenda sambamba na misingi ya vyombo vya habari pamoja na wanahabari kwa ujumla”alieleza Salum.

Aidha Salum alisema tayari serikali imekamilisha mchakato wa kuandaa Sera mpya ya habari Zanzibar na kuwatoa hofu wadau wa habari juu ya uwepo wa sera hiyo kuwa itazinduliwa muda sio mrefu.

Mwandishi wa habari mkongwe  Salim Said alieleza kuwa uwepo wa sheria bora ni muhimu katika kuwezesha mazingira bora ya waandishi wa habari  na kuwajibika kwani uhuru wa habari na haki ya kujieleza ni nguzo muhimu za utawala bora kwasababu inapelekea umma kuelea vyema kinachoendelea kati yao na kusaidia uwajibikaji na unakuza mjadala na maarifa juu ya masuala mbali mbali.

"Vyombo vya habari ni washirika wa maendeleo, kuwa na sera na sheria bora iliyo rafiki itawawezesha waandishi wa habari kuwa na mazingira mazuri na  rafiki katika  kutekeleza majukumu yao, kwani uhuru wa habari na haki ya kujieleza ni nguzo muhimu za utawala bora kwasababu inapelekea umma kuelewa vyema kinachoendelea kati yao, na kusaidia uwajibikaji na unakuza mjadala na maarifa juu ya masuala mbali mbali katka nchi" alifahamisha, mwandishi wa habari huyo mkongwe Zanzibar.

Mwandishi wa Habari kutoka Gazeti la Chanzo Najjat Omar anasema sheria za habari zikifanyiwa mabadiliko kutaongeza uwajibikaji kwa watendaji kwa sababu sharia zilizopo zinawabana sana waandishi wa habari na kupelekea kukosa kufanya kazi kwa woga Zaidi,hali inayopelekea mamlaka kukosa uwajibikaji.

“Matarajio yangu ni kuiona serikali inabadilisha sheria kandamizi na ngumu kwa waandishi wa habari ambazo zinarejesha nyuma sekta ya habari na badala yake kuweka sheria mpya zilizo rafika kwa waandishi ambazo zitapelekea kutekeleza majukumu yetu kwa ufanisi zaidi”anaeleza Najjat

 

 

 

 

 

Mwanasheria wa kujitegemea ndugu Muhammed Faki Khatib amesema kuwa kutokuwepo kwa sheria rafiki za habari kwa waandishi wa habari kutapelekea kukosa mabadiliko nchi hasa katika tasnia ya habari pamoja na kukosa maendeleo kwani sheria zilizopo hazina uhuru kwa waandishi na kupelekea kukosa uwajibikaji katika majukumu yao.

Hii inatokana na kuwepo kwa sheria ambazo hazitowi uhuru kwa watu na kupelekea kukosa uwajibikaji na uwazi kwa baadhi ya mamlaka husika,hivyo waandishi wa habari wanakosa uwajibikaji na uwezo wa kufuatilia na kuhoji utendaji wa Serekali na taasisi nyengine.

“Patakapo kuwa na sheria zilizo rafiki za habari kutapelekea kupata mabadiliko ya nchi hasa katika tasnia ya habari pamoja na maendeleo katika nchi, kwani kutakuwa na misingi bora ya sheria ambazo zinatoa uhuru kwa kila mtu, na zitapelekea kukuza uwajibikaji na uwazi wa Serekali,hivyo waandishi wa habari watapata uwezo wa kufuatilia na kuhoji utendaji wa Serekali na taasisi nyengine kwa ufanisi zaidi”ameeleza Mwanasheria.

Kwa ujumla mabadiliko ya  sheria za habari zina uwezo mkubwa wa kubadilisha tasnia ya habari kuwa chombo imara cha maendeleo ,haki na demokrasia pamoja na kuweka mazingira mazuri ya sheria ,habari zinaweza kufikishwa hadi maeneo ya vijijini na kwa makundi yasiyokuwa na sauti,kama wanawake ,watu wenye ulemavu na vijana ambapo itapelekea kupata maendeleo katika nchi na taifa kwa ujumla,hivyo basi ni vyema kwa Serekali ,wadau wa sharia,pamoja na mamlaka zote zinazohusika kuifanyia kazi sharia ya habari mpya ambayo itakwenda na misingi ya tasnia ya habari nchini.

Post a Comment

0 Comments