Ticker

6/recent/ticker-posts

Mabadiliko Ya Sheria Za Habari Na Matarajio Ya Maendeleo

 


Na Siti Ali, Zanzibar

MABADILIKO ya Sheria ya Habari yanaweza kuongeza uhuru wa kujieleza ,haki na wajibu lakini pia huenda kushughulikia tatizo la hadhi ya wanahabari, ambayo itawafanya waandishi wa habari kupewa kipao mbele na kuheshimiwa kama zilivyo kazi nyengine, pamoja na kuifanya kazi ya habari iwe taaluma muhimu,taaluma ambayo ina kipato kinachoeleweka kwa mujibu wa sheria .

Hali hii imebainika kutokana na waandishi wa habari kukosa sheria rafiki kwao na kupelekea kukosa uhuru katika kazi zao na kupelekea kukosa ufanisi wa kufanya  kazi zao.

Miradi mbali mbali inayohusu maendeleo inapatikana kutokana na vyombo vya habari, kwani hupata fursa ya kutangaza changamoto zilizopo na inapelekea maendeleo katika nchi.

Mwandishi wa Habari kutoka Gazeti la Chanzo Najjat Omar anasema sheria hizi zikifanyiwa mabadiliko kutakuwa na matarajio mazuri kwa sababu wadau wa maendeleo wataleta miradi mikubwa sana  ya nchi na serikali itapata fedha nyingi  kwa kuwa kutakuwa na uhuru wa  kulinda habari na wanahabari kwa ujumla.

“Matarajio yangu kama mwandishi wa habari kuona serikali inanipa nafasi ya kubadilisha sheria kandamizi na ngumu ambazo zinarejesha nyuma sekta ya habari”anaeleza Najjat.

Aidha Najjat amesema kuwa anatajia kuona kizazi cha sasa na kijacho kinapigania misingi ya haki ,maendeleo na kufuata sheria mpya zitakazowekwa na kufuata demokrasia pamoja na kutoona sheria kandamizi zilizopita nyuma.

“ Matarajio yangu ni kuona kizazi cha sasa na kijacho cha uandishi kinapigania  misingi ya haki ,maendeleo na kufuata sheria mpya zinazowekwa za demokrasia  pamoja na kutoona sheria kandamizi zilizopita nyuma na kuwa mashujaa katika kulinda mikataba ya haki za binaadamu,mikataba ya sheria na yote iliyosainiwa na Serekali hususani katika Serekali ya awamu hii ya nane chini ya uongozi wa Mh Rais Hussein Ali Mwinyi pamoja na waziri wa habari vijana utamaduni na michezo Mh Tabia Maulid Mwita”Najjat amesema.   

Mwandishi wa habari kutoka Daillynews  Maryam Said amesema iwapo kutakuwa na sheria rafiki za habari ,mabadiliko kadhaa chanya katika tasnia ya habari bali na jamii kwa ujumla  yanaweza kutokea ikiwemo uwazi na uwajibikaji kuboresha utendaji wa taasisi za Serekali kuimarika kwa ubora wa habari, ambapo waandishi watafanya kazi bila ya hofu ,hivyo habari zitakuwa za kina ,zenye uchunguzi ,na zenye ukweli zaidi  itapelekea mafanikio katika nchi.

“Kuwepo kwa sharia rafiki kutaleta mabadiliko chanya katika tasnia ya habari yanaweza kutokea ikiwemo uwazi na uwajibikaji pamoja na kuboresha utendaji wa taasisi za Serekali ambapo waandishi watafanya kazi bila ya hofu ,hivyo habari zitakuwa za kina ,zenye uchunguzi ,na zenye ukweli Zaidi  ambapo itapelekea mafanikio katika nchi.”ameeleza Maryam.

 Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mh Tabia Maulid Mwita wakati akizungumza na Maafisa Habari tarehe 4 Aprili katika Ukumbi wa New Amani Complex amesema katika kipindi kijacho serikali inatarajia  kuisoma pamoja na kuupitisha Mswaada wa Sheria ya Habari ambayo itasaidia kuleta mabadiliko katika nchi na taifa kwa ujumla.

“Serikali ipo katika mkakati wa kuisoma sheria mpya ya habari ya Zanzibar na tunatarajia kuipitisha na kuupeleka mswada katika Baraza la Wawakilishi ili tuweze kuipata sheria mpya yenye kuaminika itakayotumiwa na maofisa wa Habari”anaeleza Waziri Tabia.

Katibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) Mwinyimvua Abdi Nzukwi anasema kuwa wanatarajia sheria rafiki za habari zitakazokuwapo zitatoa uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko katika tasnia ya habari,tasnia ya habari kuwa kichocheo cha maendeleo,haki na demokrasia katika nchi kwani wananchi watajihisi salama kutoa maoni yao kupitia majukwaa ya habari na kupelekea ustawi wa jamii pindi watakapotoa maoni yao.

“Tunatarajia kuwapo kwa sheria rafiki za habari ambazo zitapelekea kupata mabadiliko katika tasnia ya habari, tasnia ya habari kuwa kichocheo cha maendeleo ,haki na demokrasia katika nchi kwani wananchi watajihisi salama kutoa maoni yao kupitia majukwaa ya habari na kupelekea ustawi wa jamii”anaeleza Mwinyimvua Katibu wa ZPC.

Afisa programu wa masuala ya utetezi na uchechemuzi kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA –ZNZ) Zaina Abdallah Mzee anasema kuwa wanachukua jitihada za kuzisemea sheria zote zinazohusu habari ambazo haziko huru, ili kusaidia kupata mabadiliko katika nchi, kwani kufanya hivyo kutasaidia kupatikana maendeleo kwa haraka kwani wanahabari wakifanya kazi zao vizuri Serikali itayakisi yaliyoko kwa wananchi na itapata fursa ya kufanyia kazi kwa maslahi ya nchi.

“Tunachukua jitihada ya kutetea na kufanya uchechemuzi wa sheria zilizopo za habari ambazo haziko rafiki kwa waandishi wa habari na vyombo vya habari ili zirekebishwe na tunatarajia sheria mpya  zitakazo kuwapo zitakwenda na misingi imara ya haki,wajibu,na uhuru na ulinzi kwa waandishi na vyombo vya habari ili mchango wao katika maendeleo ya nchi uonekane na utambulike ,”anaeleza Zaina.

Mwanasheria wa kujitegemea ndugu Muhammed Faki Khatib anasema kuwa kuwapo kwa sheria rafiki za habari kwa waandishi wa habari kutapelekea kupata mabadiliko makubwa nchi hasa katika tasnia ya habari pamoja na maendeleo katika nchi, na taifa kwa ujumla.

Hii inatokana na kuwepo kwa misingi bora ya sheria ambazo zinatoa uhuru kwa kila mtu ambazo zitapelekea kukuza uwajibikaji na uwazi wa Serikali,hivyo waandishi wa habari watapata uwezo wa kufuatilia na kuhoji utendaji wa Serikali na taasisi nyengine kwa ufanisi zaidi.

Patakapo kuwa na sheria zilizo rafiki za habari kutapelekea kupata mabadiliko makubwa ya nchi hasa katika tasnia ya habari pamoja na maendeleo katika nchi, na taifa kwa ujumla.

Itakapokuwapo  misingi bora ya sheria ambazo zinatoa uhuru kwa kila mtu, ambazo zitapelekea kukuza uwajibikaji na uwazi wa Serikali,hivyo waandishi wa habari watapata uwezo wa kufuatilia na kuhoji utendaji wa Serikali na taasisi nyengine kwa ufanisi zaidi”anaeleza Mwanasheria.

Kwa ujumla mabadiliko ya  sheria za habari zina uwezo mkubwa wa kubadilisha tasnia ya habari kuwa chombo imara cha maendeleo ,haki na demokrasia pamoja na kuweka mazingira mazuri ya sheria ,habari zinaweza kufikishwa hadi maeneo ya vijijini na kwa makundi yasiyokuwa na sauti,kama wanawake ,watu wenye ulemavu na vijana ambapo itapelekea kupata maendeleo katika nchi na taifa kwa ujumla.

Post a Comment

0 Comments