Na
Thuwaiba Habibu, Zanzibar
Ikiwa uhuru wa habari Zanzibar umeainishwa katika
katiba  ya mwaka(1984 ) kifungu cha  ( 18 )ya katiba ya Zanzibar inayosomeka kama
ifuatavyo.
(18) (1) Bila ya kuathiri sheria nyengine  za nchi,kila 
mtu anayo haki ya uhuru wa maoni (kujieleza).kutafuta kupokea na
kusambaza habari na mawazo yake 
kupitia  chombo chochote cha
habari  bila kujali  mipaka ya nchi  na pia anayo haki na uhuru  wa kutoingiliwa mawasiliano yake.
Kifungu hiki cha Katiba kimempa uhuru Mwandishi wa
habari  kutafuta , kupokea na kusambaza
taarifa .
Lakini kupitia Sheria mbili kuu zinazohusu masuala ya
habari; ambazo ni Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu,
Na. 5 ya mwaka 1988 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 8 ya mwaka 1997; na pia
Sheria ya Tume ya Utangazaji ya mwaka 1997 pamoja na Marekebisho yake ya mwaka
2010.ambazo zina vifungu  vinavyokinza
uhuru  huo na kupelekea waandishi kupata
changamoto kadhaa ambazo zinaathiri uhuru wa habari. kikiwemo kifungu cha 26
cha sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari 
za Magazeti na vitabu ,Na 5 ya mwaka 1997 kinavyosomeka .
"Mali  za
vyombo  vya habari zinaweza  kutaifishwa endapo vyombo hivyo vitakiuka
masharti ya sheria hii"
Kifungu hiki hakikutaja masharti ya aina gani hivyo
kinaweza kutumika wakati chombo kikitoa taarifa ambayo mamlaka hawakuipenda
basi wanaweza kukitaifisha.
Nazi haishindani na jiwe  ni msemo wa Kiswahili ambao hutoa tafsiri ya
mtoto kutoweza kushindana na mzazi wake 
lakini msemo huu umesadifu kwa Zanzibar kwasababu badala ya  katiba kuwa juu ya sheria, mtoto sheria yuko
juu ya mama yake katiba,kwasababu  katiba
imetoa ruhusa hiyo pale iliposema ; "bila ya kuathiri sheria nyengine  za nchi".
Mwandishi wa habari 
Jesse Mikofu anasema Katiba imetoa 
maelekezo  na msimamo kama
tunavyojuwa katiba ni sheria mama  lakini
kila  tulichopewa na Katiba
kimenyang'anywa .
"Hii ni sawa 
sawa na kupewa  chakula kwa mkono
wa kulia  na kunyang'anywa mkono kwa
mkono wa kushoto;Mfano ni  kifungu cha 30
cha  sheria ya Usajili wa Wakala wa
Habari za Magazeti  na Vitabu, Na 5 ya
mwaka  1997 ambayo Waziri amepewa Mamlaka
ya kufungia gazeti kwa manufaa ya umma au kwa maslahi  ya Amani na utulivu.
 Hii inatokea
kwasababu sheria haikufafanua maslahi ya umma 
na Waziri anapimaje.
Mwandishi wa habari kutoka Tiffu Tv Siti Ali anasema
sheria  ya habari ndiyo zinakwamisha
uhuru wa habari kwasababu zipo kinyume 
na katiba,na kupelekea waandishi kukosa pakuegemea na kupata
changamoto  nyingi.
"Katiba inatupa uhuru wa kupokea na kukusanya
taarifa ila sheria zetu hari zina vifungu ambazo vinakwaza uhuru wa kufanya
hivyo." alieleza.
  Mwana habari
Mkongwe na Zanzbar ambaye amekuwa mstari wa mbele kuonyesha udhaifu uliopo
katika sheria za hivi sasa, Shifaa Said Hassan,   ambaye ni afisa Mwandamizi wa Baraza  la Habari Tanzania (MTC) katika ofisi za
Zanzibar
 anasema wadau
wa habari wamekuwa wakifanya uchechemuzi 
kuwaeleza wenye mamlaka umuhimu wa kuwa na sheria mpya ya habari.
Wajumbe wa Kamati ya Wataalam wa Habari Zanzibar
(ZAMECO) wameonana na Tume ya Marekebisho ya Sheria, na Wizara ya Habari
kupeleka mapendekezo ya Wanahabari na Wadau wa Habari kuhusu mabadiliko ya
Sheria za Habari Zanzibar lakini jitihada hizo zimegonga mwamba.
Tanzania imeiridhia mikataba mingi ya kikanda na
kimataifa inayosisitiza umuhimu wa uhuru wa habari na uhuru wa kujieleza.
Mikataba hii ni pamioja na ule wa kimataifa wa haki za binadamu wa 1948 ambao
umesisitiza uwapo wa uhuru wa kujieleza kwa mataifa yote  lakini hadi wakati huu zanzibar imekosa uhuru
huo kwa sababu ya baadhi ya sheria zilizopo.
Mkufunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar (SUZA) na Mtetezi wa
Masuala ya Habari Said Suleiman anasema kuwapo kwa sheria zenye mapungufu mengi
kwa sekta ya habari kunakwaza uhuru wa kukusanya taarifa, kusambaza na hata
uhuru wa kujieleza na kutoa maoni na hivyo kukwaza maendeleo ya nchi kwa
ujumla. 
"Tumeona kuwa sheria za habari zina mapungufu
mengi ambayo yanayokwaza uhuru wa habari," anasema Said.
Mwanasheria na Mtetezi wa Masuala ya habari Juma
Khamis Juma anasema ni kweli kifungu cha 18 cha Katiba kinatoa uhuru wa habari,
lakini kama utakisoma vizuri utagundua kwamba kifungu hiki kinatoa uhuru kwa
upande mmoja na kuzuia uhuru huo kwa upande mwingine. 
"Ndio maana unakuta vifungu vilivyomo katika
sheria za habari vina nguvu zaidi kuliko kifungu cha hiki cha Katiba," 
Changamoto hii inasababisha malalamiko kwa waandishi
wa habari na vyombo vya habari. Wataalamu wa masuala ya sheria na habari,
wamekuwa wakikizungumzia kwa muda mrefu kifungu hiki cha 18  cha katiba ambacho kinatofautiana na kifungu
kama hicho kilichopo katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka
1977.
Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania
Zanzibar Dkt Mzuri Issa anasema Katiba zote mbili ya Tanzania na ya Zanzibar
zimetoa haki na  uhuru wa kujieleza
lakini kupitia Sheria za Habari tulizo nazo, suala hilo limedhibitiwa.
"Ipo haja kwa waandishi  kupata haki yao ya uhuru wa kutafuta, kutoa
maoni na kusambaza habari kwa kuwa vyombo vya habari ni daraja linalounganisha
serikali na wananchi na vyombo vya habari ndiyo mhimili mkuu wa demokrasia na
maendeleo katika nchi.
 


 
 
 
0 Comments