Ticker

6/recent/ticker-posts

Kamati Ya Siasa Kusini: Fedha Za Mfuko Wa Jimbo Zielekezwe Katika Miradi Yenye Tija Na Manufaa Kwa Jamii.



Wajumbe wa kamati ya siasa  Wilaya  ya Kusini  wameshauri  fedha  za mfuko wa jimbo  zinazotengwa kwa wabunge na wawakilishi kwa  ajili  ya  kusaidia  miradi ya maendeleo ya wananchi  kuelekezwa katika miradi michache  ambayo italeta  tija na manufaa  kwa jamiii

Wakizungumza mara baada  ya  kukagua  miradi inayotekelezwa  kupitia fedha hizo  ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya  uchaguzi  kwa kipindi cha miezi sita  kuanzia Octoba 2023 hadi machi  2024  kwa jimbo la Paje na Makunduchi

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya  ya Kusini  Bi Asha  Mzee Omar  na Mwenyekiti  Mohammed Hassan Haji  wamesema  kamati  imegundua  kuweko kwa  baadhi ya  miradi  iliyopangwa kutekelezwa katika nusu ya kota  inasuasua na mengine kushindwa  kutekelezwa  kabisa  kwa sababu ya wingi wa miradi na fedha ni  chache  hali inayopelekea  kutokamilika kwa wakati na wananchi kushindwa kunufaika na uwepo wa miradi hiyo.

Aidha  wamesema ni vyema  kwa  wananchi  wakaunga  mkono juhudi  zilizofikiwa na viongozi  wao wa majimbo  kwa kuthamini na kuitunza miradi hasa  ya maji safi na  salama kwa kuifukia miundo mbinu  ili kuepukana na madhara  mbali mbali ikiwemo magonjwa  na kuharibiwa.

Nae Kaimu Mkurugenzi Halmashauri Wilaya ya Kusini  Juma Mohammed Chande  amesema imefika wakati kwa viongozi wa majimbo kushirikiana na kamati za maendeleo kuhakikisha wanaibua miradi michache ambayo yana tija na yenye kwenda sambamba na kiwango cha fedha zinazoingizwa kwenye mfuko wa Jimbo kwa kila mwaka.

Miradi iliyokaguliwa ni pamoja na mradi wa  nyumba ya daktari Mtende, ukarabati wa banda la skuli  ya Kiongoni Makunduchi  na mradi wa maji safi na salama  Jambiani

Post a Comment

0 Comments