Ticker

6/recent/ticker-posts

ACT-WAZALENDO YARIDHIA KUSHIRIKI SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA ZANZIBAR, PIA YATOA MAPENDEKEZO KWA SERIKALI HIYO

 

Chama cha ACT-Wazalendo kimerichia kushiriki katika serikali ya umoja wa kitaifa pamoja na kuwaruhusu wateule wote wa chama hicho waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 28 na 29 mwezi Oktobar kushiriki katika vyombo vya maamuzi walivyochaguliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari huko katika ofisi za chama hicho Magomeni, jijini Dar-es-salaam katibu mkuu wa chama hicho ndugu, Ado Shaibu alisema wamefikia maamuzi mara baada ya kutafakari kwa kina juu ya mwenendo wa siasa za Zanzibar na Taifa kwa ujumla.

”tunafanya uamuzi huu kwa ajili ya maslahi ya wazanzibar,maslahi ya taifa pamoja na maslahi ya chama chetu” alisema katibu mkuu huyo

Alisema chama cha ACT-Wazalendo kilifanya ziara katika maeneo mbalimbali na Zaidi katika maeneo ambayo yaliathirika kwa kiasi kikubwa katika uchaguzi mkuu ili kusudi kusikiliza maoni yao juu ya suala la kushiriki au kutokushiriki katika Serikali ya umoja wa kitaifa visiwani Zanzibar ambapo asilimia kubwa ya wanachama waliridhia chama hicho kushiriki katika Serikali hiyo pamoja na kuwaruhusu wateule wote wa chama hicho ambao ni wabunge,wajumbe wa baraza la wawakilishi pamoja na madiwani kuzitumikia nyadhifa walizochahuliwa.

”tumepata muda mrefu wa kufanya tafakuri ya kina lakini pia kamati kuu imekwenda kuwasikiliza wanachama hasa katika maeneo ambayo wamepata madhila makubwa katika uchaguzi huu juu ya jambo hili ambapo  wameridhia tuwaruhusu wawakilishi wetu washiriki katika vyombo vya uwakilishi na pia tushiriki katika Serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar” aliongezea ndugu Ado Shaibu

Aidha katika hatua hio chama cha ACT-Wazalendo wameiomba Serikali ya kitaifa itakayoundwa kutekeleza mambo mbalimbali ikiwemo kufanyika kwa uchunguzi wa matukio yote yaliyotokea kabla, wakati na baada ya uchaguzi ya uvunjaji wa haki za binaadamu na kuwafariji waathirika wote pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika kupanga na kutekeleza matukio hayo, Kunafanyika Mabadiliko ya mfumo wa Uchaguzi Zanzibar ili kurejesha imani ya wananchi juu ya uwepo wa uchaguzi huru na wa haki.

Pamoja na Kunafanyika Marekebisho ya uendeshaji wa vyombo vya Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili vifanye kazi kwa Weledi na bila ubaguzi wa kisiasa.

 

Dhima ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar kwa maslahi ya Wananchi inapaswa pamoja na mambo mengine ihakikishe kuwa, inachunguza wa matukio yote yaliyotokea kabla, wakati na baada ya Uchaguzi ya uvunjaji wa haki za binaadamu, unafanyika na kuwafariji waathirika wote pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika kupanga na kutekeleza matukio hayo” Alisisitiza katibu mkuu huyo

 

Ikumbukwe kuwa katika uchaguzi mkuu wa 2020 chama cha ACT-Wazalendo kilipata asilimia 19.87% ambapo kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar kinaruhusiwa kupendekeza jina la makamu wa kwanza wa Raisi wa Zanzibar.

 


Post a Comment

1 Comments