Ticker

6/recent/ticker-posts

Pondeza Asisitiza Kukithirisha Ibada Mwezi Huu Wa Ramadhan

 


Mbunge Wa wananchi wa Jimbo la Chumbuni  Ussi Salum Pondeza amejumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika ibada ya Sala ya Ijumaa Chumbuni Bamita.

Baada Ya Sala hiyo Pondeza Aliwasihi Waumini Kuungana kwa Pamoja kwa Kuendelea Kufanya ibada jambo litakalosaidia kupata radhi za Mwenyezi Mungu.

“Malipo ya ibada zetu kwenye mwezi huu ni mara dufu ya malipo katika miezi mingine hivyo niwaombe tujitahidi kufanya ibada kwa wingi” Alisisitiza

Aidha Mbunge huyo aliushukuru Uongozi wa Wa Msikiti Wa Bamita Kwa Kuendelea Kuwapa Taaluma Ya Dini Ya kiislamu Jamii Ya Maeneo Hayo Kwa kuwafundisha Qur- an Watoto na watu wazima.

Kwa upande wake  Diwani Wa Wadi Ya Chumbuni Ambar Ujudi Bamba aliwataka waumin Wa Maeneo Hayo Kuendeleza Amani Utulivu Na Upendo.

“Endapo tutaimarisha amani na upendo miongoni mwetu itakuwa njia ya kuridhiwa na Mwenyezi Mungu na Kupiga hatu za maendeleo” Alisema

Post a Comment

0 Comments