Ticker

6/recent/ticker-posts

“Tumepanga Kusimamia Wazee Wasio Na Vyeti Vya Kuzaliwa Kupata Vyeti Hivyo” Waziri Pembe



Na Ahmed Abdulla:

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kuratibu Pencheni jamii kwa kushirikiana na taasisi mbali mbali wakiwemo Wizara ya Nchi (OR) Fedha na mipango na kusimamia wazee wasio na vyeti vya kuzaliwa ili kuhakikisha na wanapata vyeti hivyo na jambo litakalowasaidia kupata fursa mbalimbali.

Hayo yalielezwa na waziri wa wizara hiyo Riziki Pembe Juma huko ofisini kwake Kinazini, Zanzibar wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu siku ya wazee duniani itakayoadhimishwa Oktoba 01, katika ukumbi wa Dkt. Ali Mohammed Sheni – SUZA ambapo Mgeni ramsi anatarajiwa kuwa Raisi wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt. Hussei Ali Mwinyi.

Aidha alisema katika sherehe hizo wazee 25,000 waliofikia umri wa miaka 70 na kuendelea,watapatiwa vitambulisho vitakavyowasaidia katika kupata huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo kupokea pencheni jamii, kupata huduma za afya, kuingia katika viwanja vya michezo vya Serikali pamoja na kutumia usafiri wa daladala bure.

“Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepanga kutoa vitambulisho 25,000 kwa wazee wote waliofikia umri wa miaka 70 na kuendelea, ili viweze kuwasaidia katika kupata huduma mbali mbali za kijamii ikiwemo kupokea pencheni jamii, kupata huduma za afya, kuingia katika viwanja vya michezo vya Serikali, kutumia usafiri wa daladala bure, nk.” Alisema Waziri Pembe

Alifahamisha kuwa wizara itaendelea kuimarisha hali za wazee hao ikiwa ni pamoja na kuwapima maradhi mbalimbali mara kwa mara ili kuchukuwa hatua pale mabapo itatokea mmoja wapo atakutwa na ugonjwa wowote hivyo kupitia maadhimisho hayo wizara imeandaa wataalamu wa afya watakao huduma za vipimo vya maradhi mbalimbali bure kwa wazee na wananchi wote.

“Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeandaa wataalamu wa afya ili wazee na wananchi wote waweze kupimwa afya zao bure kwani afya bora ndio mtaji” Aliongezea

Kila ifikapo Oktoba 01, dunia huadhimisha siku ya wazee duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Uthabiti wa Wazee kwenye Dunia yenye Mabadiliko”

  

 


Post a Comment

0 Comments