Ticker

6/recent/ticker-posts

Madaktari Wa Afya Ya Uzazi Zanzibar Wahitaji Kupigwa Msasa

 


Na Nafda Hindi, Zanzibar

Madaktari nchini wametakiwa kutoa huduma bora kwa jamii ili kupunguza idadi ya vifo kwa watoto na mama wajawazito.

Ushauri huo umetolewa na wanawake ambao ndio walengwa wakuu wa kupokea huduma za Afya ya Uzazi kutoka maeneo tofauti visiwani Zanzibar ambapo  wamesema katika vituo vinavyotowa huduma hizo bado kunahitaji nguvu za ziada kwa madaktari wanaoshughulikia huduma ya afya ya uzazi.

Wamesema kuna changamoto kadhaa ambazo zinajitokeza wakati wa kupokea huduma ikiwemo uelewa mdogo kwa madaktari kuhusiana na afya ya uzazi jambo ambalo huleta shida kwa wanawake endapo watajiunga na moja ya huduma hizo wakati wa kutumia.

“Huduma za Afya ya Uzazi Zanzibar bado ni kikwazo hawa madaktari wenyewe yawezekana hawana Elimu sahihi juu ya afya ya uzazi, kwa mfano Uzazi wa mpango, huangaliwi Afya yako, Uzito wako na kushauriwa njia ipi sahihi utumie kwa mujibu wa Afya yako unajikuta unapewa vidonge au sindano kumbe haviendani na afya yako  hivyo baadae vinaleta matatizo,”walisema wananchi.

Mapema Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Dk Said Khamis akiwasilisha ripoti ya Afya ya uzazi amesema “chanagamoto ni nyingi kwa jamii kuhusu Afya ya uzazi kwa sababu inaonekana Zanzibar hakuna wataalam wa Afya ya uzazi,” alisema Dk Said.

Dk Said amesema waandishi wa habari nao wana uelewa mdogo kuhusu Elimu ya Afya ya uzazi Zanzibar ipo haja kwa Serikali na Mashirika binafsi kuekeza nguvu katka masuala haya na kuwapatia mafunzo waandishi wa habari kwa lengo la kuelimisha jamii.

“Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa unaonesha kwamba 60% ya vyombo vya habari Zanzibar hakuna vipindi vinavyohusu Afya ya Uzazi,” Dk Said alisema.

 Kwa upande wao waandishi wahabari wamekiri kuwa hawana  uelewa mzuri juu ya masuala yanayohusu Elimu ya afya ya uzazi hivyo wameomba kupatiwa mafunzo ya mara kwa mara  waielimishe jamii kwa usahihi kupitia vyombo vya habari kwa kutayarisha vipindi pamoja na makala.

“Tunauelewa mdogo kuhusu Elimu ya afya ya uzazi kwa sababu sisi tunaelimisha jamii kupitia vyombo vya habari tutakapokuwa na Elimu sahihi na jamii itajifunza kitu kupitia kwetu, sasa tunahitaji kupatiwa mafunzo juu ya suala hili,” waandishi wahabarin walisema.

Afisa anaeshughulikia Mradi wa Afya ya Uzazi kutoka TAMWAupande wa Zanzibar Zaina Abdalla Mzee amesema changamoto ni nyingi kuhusu Afya ya Uzazi hivyo waandishi wahabari wana kazi ya ziada na kuhakikisha wanatoa Elimu kwa usahihi kwa kutumia takwimu na kuwafuata wataalam.


Post a Comment

0 Comments