Ticker

6/recent/ticker-posts

Wanawake Zanzibar Mguu Sawa Uchaguzi 2025



Na Nafda Hindi


Wanawake wenye nia ya kugombea nafasi za Uongozi wameaswa kutovunjika moyo licha ya matatizo kadhaa wanayokumbana nayo katika kufikia malengo waliyokusudia.

Akizungumza na wanawake kutoka vyama mbali mbali vya siasa mratibu kutoka TAMWA Maryam Ame Choum amesema wanawake kwa sasa wamewawezesha wanawake zaidi ya thamannini kutoka Unguja na Pemba kwa kuwapa mafunzo ya kuwajengea uwezo katika kugombania nafasi za Uongozi.

Mapema Katibu Mwenezi CCM Khamis Mbeto amesema wanawake wana uwezo wa kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja hivyo wapewe nafasi za Uongozi kwa kuzingatia vigezo na utendaji wao wa kazi.

“Chama cha Mapinduzi kinatambuwa uwezo wa wanawake katika utendaji wao na mfano mzuri ni Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na anafanya vizuri , kwa kweli wanawake wapewe nafasi kwa kuzingatia uwezo, sifa na vigezo”, alisema.

Nae Katibu Mkuu CHADEMA Taifa Salim Mwalim amesema kwa sasa wakati umefika kuongeza idadi ya wanawake katika ngazi za maamuzi bila kuathiri mila,silka na utamaduni wa Mzanzibari.

“Wanawake kiwango chao cha uaminifu ni kikubwa ukilinganisha na wanaume, hivyo tunaweza kuwa na viongozi wanawake na tukalinda mila,silka na desturi ya Mzanzibari,”alisema.

Halima Ibrahim kutoka chama cha ACT Wazalendo amesema wanawake wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kadhaa wakati wakugombea nafasi za uongozi ikiwemo rasilimali fedha hivyo amewaomba wanawake wenye nia ya kugombea washirikiane kwa pamoja kwa lengo la kumkombowa mwanamke.

“Wanawake wenzake tunakabiliwa na changamoto kadhaa katika haya mambo hivyo wasia wangu kwangu tuungane pamoja ili kumkombowa mwanamke bila kuangalia itikadi za vyama.ukabila,rangi,dini wala mtu alipotoka,”alisema.

Nao washiriki wa mkutano huo wamesema katika kufikia ngazi za maamuzi kuna matatizo kadhaa wanayokutana nayo ikiwemo mfumo uliwekwa katika vyama vya siasa na jamii kutokubadilika kwa kuwa na dhana potofu kuwa mwanamke hawezi kuongoza.


Post a Comment

0 Comments