Ticker

6/recent/ticker-posts

Bonanza La Polisi Jamii Laja Na Ulinzi Jirani

 



JESHI la polisi wilaya ya Kusini imedhamiria kuimarisha hali ya ulizi na usalama wilayani humo kwa kuwashirikisha wanajamii ili kufikia lengo la kukataa uhalifu kwa kila mwananchi.

Dhana hiyo imekuja kuongezwa kazi na kampeni maalumu ya ulinzi JIRANI ambayo itasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti uhalifu ikiwemo makosa ja jinai.

Wakitoa ufafanuzi juu ya kampeni hiyo katika viwanja tofauti  Inspekta Msaidizi wa Polisi Kulwa na Inspekta wa Polisi ambaye pia ni Mratibu wa Bonanza hilo Mtumwa Mussa Khamis wamesema ni Hali ya mwananchi kulinda eneo lake na la jirani yake Ili lisifanyiwe uhalifu.

Wamesema endapo majirani hawatoshirikiana katika ulinzi kuna uwezenano mkubwa kufanywa uharibifu wa  Mali hivyo wametoa wite kwa majirani kutekeleza dhana hiyo ya ulinzi katika kuweka usalama wa mali zao.

Ikumbukwe wiki iliyopita Mratibu wa bonanza hilo Inspekta wa polisi Mtumwa kwenye kipindi cha Zenj Sports kinachorushwa hewani na kituo cha Redio cha Zenj FM alisema lengo kuu la bonanza hilo ni kutoa elimu kwa vijana juu ya kujiepusha na makosa ya jinai.

Matokeo ya michezo ya leo:

Uwanja wa Kibuteni

Kizimkazi Dimbani 0-0  Mtende

Uwanja wa Jamuhuri Makunduchi

Nganani 4-1 Kibuteni

 

Ratiba ya michezo ya Kesho:

Uwanja wa Kibuteni

Muyuni “B” VS Kajengwa

Saa 10:00 Alaasiri

Uwanja wa Jamuhuri

Kizimkazi Mkunguni VS Kijini

Saa 10:00 Alaasiri

Post a Comment

0 Comments