Ticker

6/recent/ticker-posts

Wasanii Wasema Sheria Inayolinda Uhuru Wao Ni Lazima Kwa Maslahi Ya Taifa

 


Na Ahmed Abdulla:

Wasanii mbalimbali nchini wamesema kuna kila sababu ya kupantikana kwa uhuru wa kweli wa kujieleza na kupaza sauti za kupinga ukandamizaji wa haki za wengine ili kupata maendeleo ya kweli nchini.

Wameyasema hayo kwa nyakati tofauti kufuatia kutokuwepo kwa uhuru wa kweli katika kuyasemea yale yanayowakandamiza watu wa jamii za chini hali inayohatarisha kuwakosesha haki miongoni mwa jamii za watu hasa wa tabaka la chini.

Abeid Nasib ni muandishi wa filamu kutoka Zanzibar amesema uhuru wa kujieleza katika sekta ya filamu haupo kwani maisha halisi ya Zanzibar yanaleta ukakasi juu ya filamu na ukizingatia kuwa filamu ina uwanja mpana.

“Filamu ina uwanja mpana hivyo unaweza kuzungumzia vitu vinavyofanyika Zanzibar lakini ukaambiwa filamu yako imekwenda kinyume na tamaduni” amesema  Abeid

Nilipomuuliza kuhusu uhuru wa kutoa filamu za kukosoa hapo ndio alisisotiza kuwa haupo kwani ukiangalia tokea enzi za mababu kuna mengi ambayo yametokezea lakini watunzi wa filamu wameshindwa kutunga filamu zenye mnasaba wa mambo hayo.

“Kuna mikasa mingi ya siasa iliyojitokeza ya hata watu kutokuzikana,kuchomeana moto nyumba kwa baadhi ya jamii, ugomvi wa wavuvi wa jamii moja na nyingine lakini haijawahi kuandikwa filamu ya mambo hayo hivyo inaonyesha uhuru haupo kabisa” aliongezea

Amesema licha ya hayo lakini bado anayo nia ya kuandika filamu zinagusa maisha halisi ya  Zanzibar na yale yanayotendeka huku akiwaambia waandishi wenzake kuwa ili kuleta mabadiliko ya jambo lolote baya basi kuna kila sababu ya kuyaandikia filamu ili yaonekanwe na jamii nyingine ili yaweze kuachwa.

 

“Sanaa zinahitaji mambo yanayogusa mioyo ya watu bila kujali watendaji wataumia kiasi gani kutokana na kuyazungumza mabaya yao” alimalizia Mwandishi huyo

Bakar Hamad Abdalla kwa jina la sanaa ni Beka-h yeye nimsomaji wa nasheed kutoka kisiwani Pemba amesema bado uhuru wa kujieleza umekuwa ni changamoto katika jamii za kizanzibari kwani aliwahi kutoa kazi inayozungumzia siasa tu kwa ujumla wake lakini baabdi ya vyombo vya habari walihofia kuicheza.

“Niliwahi kutoa kazi inayozungumzia siasa ila baadhi ya vyombo vya habari havikucheza kazi hiyo na nadhani ni hofu tu ndio ilifanya wasiicheze” alisema Beka-h

Amesema licha ya changamoto hiyo lakini haikumfanya ahofie kutoa kuandaa kazi zinazozungumzia uhalisia wa maisha halisi ya Zanzibar ambapo kwa sasa anaandaa kazi nyingi zenye kugusa changamoto za wazanzibari.

“Wijahofia bado nitaendelea kutoa kazi nyingi tu zinazozungumzia maisha halisi ya Zanzibar na changamoto za wazanzibar” aliongezea

Hata hivyo amewaoma wasanii wenzake na wote wenye sauti ya kuzunguma wasemee changamoto na kadhia zinazowakabili wananchi ili wenye dhamana ya maeneo hayo waweze kuwajibika.

Nae msanii wa zenji Fleva Misheli Santiago (Misheli Tz) naye pia amesema uhuru wa kutoa sanaa inayokosoa watu wa tabaka la juu haupo na ukizingatia Zanzibar kuna matukio mengi ambayo si ya kawaida.

Amesema watu watabaka la juu wao wanahitaji nyimbo sa kusifia tu huku watu wa tabaka la chini wao wakihitaji nyimbo zinazowakosoa viongozi pale wanapokengeuka.

“Nyimbo zenye soko ni zile za kukosoa mabaya ya watu Fulani lakini changamoto ni kwamba watu wa tabaka la juu wao hutaka nyimbo za kusifia tu” amesema Msanii huyo

Hivyo amesema waziri mwenye dhamana anatkiwa ahakikishe uhuru wa wasanii ili kufanya kazi kwa mapana zitakazogusa maisha halisi ya wazanzibar.

“Waziri mwenye dhamana atuhakikishie uhuru na usalama wetu ili tufanye kazi zenye kuibua changamoto na kadhia za wananchi” amemalizia

Hata hivyo wasanii hao wamesema wanalazimika kutoa maudhui ya jamii nyingine na kuziacha jamii zao ambazo zina mikasa mingi ya kusisimua ambayo inahitajika kutolewa maudhui.

Post a Comment

0 Comments