Ticker

6/recent/ticker-posts

Wazazi Waaswa Kutokata Tamaa Kesi Za Udhalilishaji


 

Na Ahmed Abdulla Othman

Wazazi na walezi visiwani Zanzibar wametakiwa kutokata tamaa na kupambana iwapo watoto wao watakutwa na kadhia ya kudhalilsihwa ikiwemo kubakwa au kulawitiwa.

 

Wito huo umetolewa na miongoni mwa mzazi ambae jina lake nilanhifadhiwa kufuatia kadhia ya mtoto wake kubakwa na kukashifiwa na mtu aliedai alikua karibu nao.

 

Alisema kwa kuwa mtu aliembaka mtoto wake alikua mtu wa karibu walimrubuni mume wake na alikua  tayari kufuta kesi hio baada ya kupewa shilingi milioni nne.

 

Alisema watu hao bila ya hofu walimshawishi mume wake na kumpa fedha ili kesi hio waiondoe kituo cha polisi lakini yeye binafsi alikataa kufanya hivyo na kuendelea kupambana.

 Alieleza kuwa watu hao walimpa mume wake shilingi milioni nne lakini yeye alikataa kuchukua pesa hio na kupelekea kutofautiana na mume wake lakini hakujali kwani aliamini anapambania utu wa mtoto wake na si jembo jengine lolote lile.

Akiendelea kusimulia zaidi mama huyo huku machozi yakimtoka alisema ni jitihada zake binafsi na ushauri aliokua akipata kutoka kwa maafisa wa TAMWA-ZNZ kila wakati ndio faraja pekee iliomfanya kutokata tamaa.

Sambamba na hayo alieleza kutokana na kufuatilia kesi hio bila kuchoka hatimae Mahakama ilimtia hatiani aliemfanyia unyama huo mtoto wake na kumuadhibu kwenda chuo cha mafunzo kwa miaka 30.

Mama huyo anaamini kuwa hayo yote yametokana na jitihada binafsi ambazo wazazi wengine wanapaswa kuwa nazo na sio kukata tamaa wakiamini kuwa hakuna hukumu itakayotolewa.

Post a Comment

0 Comments