Ticker

6/recent/ticker-posts

"Kamati zenye dhamana ya kusimamia miradi ya maendeleo shirikianene kuondoa changmoto za wananchi" Thuwaiba Jeni







Kamati Za wananchi zilizopewa dhamana Ya kusimamia Miradi ya maendeleo Katika majimbo zimetakiwa kuweka utaratibu wa kusaidana yanapotokea matatizo Ili kuhakikisha wanatoa Huduma nzuri kwa wananchi.

 

 

Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii ambae pia ni diwani wa kuteuliwa manispaa ya  Magharibi b,  Thuwaiba Jeni Pandu,alipokua katika ziara yake ya kusikiliza kero zinazowakabili wananchi wa shehia ya Pangawe wilaya ya magharibi B.

 

Amesema lengo la kufanya ziara hiyo ni baada kupekea  malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kukosa huduma ya maji safi na salama kwa muda mrefu jambo linalo walazimu kutumia gharama nyingi kununua maji jambo linalodumaza hali za kiuchumi kwa wananchi hao.

Aidha amewataka wananchi kuwa nasubra katika kipindi hichi kwani viongozi wa Jimbo watahakikisha wanatatua tatizo hilo ili kuona furaha za wananchi hao zinaimarika. 

 

Sambamba na hayo amesema viongozi wamekua wakijitahidi kuhakikisha wanaondoa changamato   ikiwa ni pamoja na kujenga visima hivyo ni vyema kwa wanakamati kuwajibika ipasavyoa ili kuondolea usumbufu wanaopata wananchi ikiwa ni kuhakikisha kuwa huduma zote za kijamii zinakuwa imara katika maeneo yao.

 

Nao wanakamati  wamesema tatizo kubwa lilopo ni baadhi ya wananchi kushindwa kulipa ada hali inayo pelekea kushindwa kufanya matengenezo pale linalopo tokezea tatizo katika miundombinu ya maji.


Post a Comment

0 Comments