Ticker

6/recent/ticker-posts

"WAJASIRIAMALI MUNA MCHANGO MKUBWA KATIKA MAENDELEO YA TAIFA" GEOFREY MWAMBE

Waziri mteule wa Wizara ya Viwanda na Biashara na Mbunge wa Masasi, Mhe. Goodfrey Mwambe (shati ya bluu bahali) akipata maelezo ya bidhaa zinazozalishwa kutoka kwa mjasiliamali mdogo



Kuwepo kwa wajasiriamali wengi katika taifa ndipo kunakopelekea maendeleo endelevu hususan katika sekta ya viwanda na biashara nchini.

Hayo yalielezwa na waziri mteule wa wizara ya viwanda na biashara Mhe, Geofrey Idelphonce Mwambe alipotembelea maonyesho ya tano ya bidhaa za viwanda vya Tanzania yanayoendelea huko katika uwanja wa maonyesho wa Mwl J.K.Nyerere (SabaSaba).

Alisema serikali ya Tanzania inathamini juhudi za wajasiriamali kwani wana mchango mkubwa wa kuleta maendeleo chanya ktika taifa Zaidi katika Nyanja ya ajira hivyo aliwahakikishia kufanya nao kazi pamoja na kuwaandalia mazingira wezeshi ili kusudi waendelee na majukumu yao bila ya kuwepo na changamoto.

“serikali itaendelea kuwapa msukumo ili tuone jitihada zenu katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi yanafanikiwa” alisema mteule huyo



Waziri mteule wa Wizara ya Viwanda na Biashara na Mbunge wa Masasi, Mhe. Goodfrey Mwambe (shati ya rangi buluu bahari) akipata maelezo ya bidhaa kutoka kwa afisa wa kiwanda cha Kahawa (Mbinga Coffee) 


Alisema kuwa lengo la kutembelea Maonesho hayo  ni kujifunza, kujionea bidhaa zinazozalishwa na viwanda vyetu vya ndani, kujua bidhaa zinavyotengenezwa, aina ya bidhaa hizo na kufahamu upatikanaji wa malighafi pamoja na kujua muunganiko wa uzalishaji na upatikanaji wa masoko kwa bidhaa hizo.   

“Nimepata faraja kuona mwamko mkubwa wa Watanzania kuweza kuzalisha bidhaa za Tanzania ambapo awali bidhaa hizo tulikuwa tunaagiza kutoka nje ya nchi, kupitia Maonesho nimeona dhamira yao na imenipa somo la kuona uhitaji wa uzalishaji mkubwa ili kuweza kusafirisha nje ya nchi” amesema Mhe Mwambe


Waziri mteule wa Wizara ya Viwanda na Biashara na Mbunge wa Masasi, Mhe. Goodfrey Mwambe (shati ya bluu bahali) akipata maelezo ya bidhaa zinazozalishwa kutoka Chuo kikuu cha Dar es salaam wakati alipotembelea Maonesho ya Tano ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania yaliyoanza tarehe 3 -9 Desemba

 

Aliongezea kuwa nchi ya Tanzania  imeingia kwenye uchumi wa kati, hivyo wajasiriamali wakiwezeshwa kwa kupata kipato kikubwa, wastani  wa mapato utaongezeka na kuwa juu hivyo juhudi ya pamoja ndani ya serikali kuelekea mwaka 2025 nchi itaingia kwenye uchumi wa kipato cha juu utakaopelekea kuboresha maisha ya Watanzania na kutengeneza uchumi wa viwanda ulio imara pamoja na wenye muunganiko mzuri kati ya wajasiriamali wa kilimo, mifugo, uvuvi, viwanda na masoko .

  

Post a Comment

0 Comments