Ticker

6/recent/ticker-posts

MATAPELI WATUMIA JINA LA WAZIRI MKUU KUTAPELIA WATU

 

WANANCHI wametakiwa kuwa na tahadhari kuhusu ujumbe unaosambazwa kwenye mtandao wa Facebook unaotumia jina la ‘Waziri Mkuu Kassim Majaliwa’ ukiwataka wajasiriamali watume pesa ili wapewe mkopo na taasisi iliyojitambulisha kama Kassim Majaliwa Foundation, kwani mtandao huo ni batili.

 

Katika taarifa iliyotolewa leo Dicemba 8 na Ofisi ya waziri mkuu kwa vyombo vya habari  ilieleza kuwa Ujumbe huo unawataka wananchi watume namba za vitambulisho vya kupiga kura ili waweze kupatiwa mkopo anaotaka mkopaji ndani ya saa 24 kwa kutumia namba ambayo imesajiliwa kwa jina la Yunus Milanzi.

 

Kufuatia kuwepo kwa kadhia hiyo Ofisi ya Waziri Mkuu imekanusha kuwepo kwa taasisi hiyo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa hahusiki na Taasisi yoyote ya utoaji wa mikopo.

 

Aidha taarifa imeendelea kusema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu inafuatilia suala hilo kwa karibu ili kuwabaini wahusika wa utapeli huo ili hatua kali za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

 

 


Post a Comment

0 Comments