Ticker

6/recent/ticker-posts

Mamlaka Zinakwama Wapi Marekebisho Ya Sheria Za Habari Zanzibar?

 

Na Ahmed Abdulla, Zanzibar:

Ikiwa ni takriban miaka 20 sasa wadau wa sekta ya habari wakipaza sauti juu ya uwepo wa sheria za habari ambazo zinakandamiza uhuru wa waandishi wa habari na vyombo vya habari.

Miaka yote hiyo bado hakujapatikana muafaka kutoka kwa serikali juu ya upatikanaji wa sheria mpya jambo lanaloendelea kudumaza ufanisi wa vyombo vya habari kwani hakuna uhuru wa moja kwa moja kwa vyombo hivyo.

Miongoni mwa sheria hizo ni ile  Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu Na. 5 ya mwaka 1988 na Sheria ya Tume ya Utangazaji Na. 7 ya mwaka 1997.

Miongoni mwa vifungu vyenye  utata katika Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu Na. 5 ya mwaka 1988 kifungu cha 27 (1) ni pale inapompa mamlaka Afisa wowote wa jeshi la polisi kukamata gazeti lolote, popote linapopatikana ambalo limechapishwa au anashuku limechapishwa habari kinyume na sheria hii.

Dkt. Mzuri Issa ni Mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Upande wa Zanzibar TAMWA-ZNZ alizisisitiza mamlaka zinazohusika na marekebisho ya Sheria kuharakisha mchakato wa sheria za habari ili kupatikana kwensheria mpya za habari zinandolinda uhuru wa habari.

“Endapo itapatikana sheria inayotoa uhuru wa habari itaisaidia serikali kupiga hatua za maendeleo kwani waandishi wataandika habari zinazogusa uwajibikaji lakini pia wananchi watanufaika kupata habari zenye uzito zenye kuibua mambo mbalimbali yenye tija kwa taifa” alisema Dkt. Mzuri

Mwandishi kutoka kwa Mtandao wa The Chanzo Najat Omar amesema kuwepo jwa sheria ambazo si rafiki wa waandishi wa habari kunaweza kuchochea ufisadi katika taifa kwani waandishi watakuwa na hofu ya kuandika habari hizo kwa kuhofia usalama wao.

“Athari kubwa zaidi ni kutokuwa na taarifa sahihi sababu waandishi wataandika habari za kupongeza zaidi na kushukuru tu” alisema

Kwa upande wa Mwandishi wa habari mkongwe visiwani Zanzibar Salim Said alisisitiza kwamba vyombo vya habari havina nia mbaya kwa Serikali bali ni washirika muhimu katika kuleta maendeleo kwa jamii huku akisema kuwa upatikanaji wa sheria inayotoa uhuru kwa vyombo vya habari ni muhimu.

Je kwa miaka hiyo serikali imefikia wapi juu ya marekebisho ya habari hizo?

Mnamo May 03, 2023 katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa Vyombo vya habari diniani Rais Dk. Mwinyi, alizungumzia mchakato wa marekebisho ya sheria ya Habari, ambapo alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tayari imeandaa mswada wa sheria hiyo yenye madhumuni ya kufuta Sheria iliyopo ya Usajili wa Magazeti, Wakala wa Habari na vitabu Sheiria nambari 5 ya mwaka 1988 ambapo marekebisho yake ni sheria nambari 8 ya mwaka 1997 na kutunga Sheria mpya ya Huduma za Habari na Mambo yanayohusiana na hayo.

Dk. Mwinyi alieleza kwamba Mswada huo tayari uko Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na unatarajiwa kutoa sheria nzuri itakayohusiana na masuala ya habari.

Lakini hayo yakiendelea lakini hadi leo mswaada huo haujajuulikana ni lini utakuwa sheria rasmi.

Hivyo ni jambo la kufurahisha kuona kila mmoja kwa nafasi yake anatekeleza wajibu wake ili kuona mswaada huo unakuwa sheria.

Post a Comment

0 Comments