Ticker

6/recent/ticker-posts

Vijana Na Wanawake Wamwilikiwa Tochi Kwenye Kilimo

 


 Na Nafda Hindi:

Mkurugenzi wa  Chama  cha Waandishi wahabari Wanawake Tanzania Zanzibar Dk Mzuri Issa Ali amewaomba  vijana na wanawake kuzidisha bidii katika kilimo kwa lengo la kujikwamua na umaskini na kuleta maendeleo katika Taifa.

Akitembelea mabanda ya maonyesho yanayomilikiwa na mradi wa VIUNGO katika siku ya wakulima Zanzibar (nane nane) huko Dole amesema kilimo ni sekta moja wapo iliodharauliwa kwa miaka mingi na sasa inaonekana umuhimu wake kwa kuongeza ajira kwa vijana pamoja na wanawake.

Aidha amesema wanawake awali wakitumia fursa ya kilimo kwa ajili ya chakula cha nyumbani pekee kwa sasa hali imebadilika na kutumia fursa hiyo kama njia moja ya kujiongezea kipato kwa ajili ya biashara.

Nae mwenye dhamana ya masoko katika mradi wa VIUNGO Zulfa M’bwana amesema lengo kuu la mradi huo ni kuongeza thamani ya vidhaa za mboga mboga, matunda na viungo pamoja na kuwaunganisha wanunuzi,wasafirishaji,wahifadhi na wakulima kwa urahisi jambo ambalo limesaidia kupata soko la uhakika ndani na nje ya nchi kama vile falme za Kiarabu katika nchi ya Oman na bara Ulaya nchini Ujerumani.

Mfanyakazi kutoka mradi wa VIUNGO Ali Said Juma  amesema wameshiriki katika maonyesho hayo kwa lengo la kutoa Elimu kwa wakulima kwa kulima kilimo bora kinachohimili mabadiliko ya Tabia ya nchi kulingana na mazingira ya nchi husika.

Mkulima ambae ni mnufaika wa mradi wa VIUNGO Aviwa Ali Songoro ameanza na kilimo cha vanilla na hatimae kuchanganya na kilimo cha migomba kwa muda wa miaka mitatu ambapo kwa sasa ana miche ya zao la vanilla isiopungua elfu moja (1000) na miche ya migomba isiopunguwa elfu tatu katika shamba lenye ukubwa wa ekari tatu.

Mkulima Aviwa ananufaika na mradi huo kwa kujikimu kimaisha pamoja na familia yake kwa kusomesha watoto na anawasihi wanawake na vijana watumie fursa ya kilimo kibiashara kwa lengo la kupiga hatua kimaendeleo na kubadilisha maisha yao.

Mradi wa VIUNGO unatekelezwa na Taasisi Tatu ambazo ni TAMWA Zanzibar. PEOPLE DEVELOPMENT FORUM,(PDF) COMMUNITY FOREST PEMBA (CFP) Unaosimamiwa na Wizara ya Kilimo,Umwagiliaji na Mifugo chini ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya(Uropean Union).

 

Post a Comment

0 Comments