Ticker

6/recent/ticker-posts

Mradi Wa Viungo Ulivyoinua Uchumi Wa Wakulima Wadogowadogo Zanzibar

 


Na Ahmed Abdulla:

ZAIDI ya wakulima 21,000 wanatarajiwa kunufaika na mradi wa viungo chini ya usimamizi wa Agri-connect ambapo unalenga kuwaelimisha wakulima ili kuongeza uzalishaji katika maeneo Yao na kumfanya mkulima aweze kulima kilimo Cha biashara na kujikwamua na umasikini.

Katika wakulima hao 21,000 watakaonufaika na mradi huo watu zaidi ya 16,000 wameshaanza kunufaika hadi inayoifanya idadi hiyo kukaribia nusu na robo ya malengo.

Wakati wakulima hao zaidi ya 16,000 wakiendelea kupatiwa mafunzo na nyenzo mbalimbali jee maendeleo ya kilimo chao yakoje na jee yameanza kubadilisha hali za maisha yao.

Vua Ali Songoro ni mkulima ambaye amenufaika na mradi wa viungo ambapo amesema mradi huo umempa manufaa makubwa kutoka kilimo cha mazoea na sasa kulima kilimo chenye tija.

“nilikuwa nimekaa nyumbani kama mkulima wa kawaida lakini baada ya Mradi huu kupitia kwa Chama cha Waandishi habari wanawake TAMWA-ZNZ walinishauri tusaidiane kwenye kilimo nikakubali na sasa najivunia kilimo ndio kinaniendeshea maisha yangu” alisema mkulima huyo

Mradi wa kilimo haukujikita tu kwenye wakulima bali hata wasarifu bidhaa za kilimo ambapo mwandishi wa habari hizi alikutana na Saida Mohammed Shaib anayejishugulisha na usindikaji wa bidhaa ambapo alisema mafunzo ya mara kwa mara juu ya shughuli zake yamemjenga kuwa na ujasiri wa kupambana licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kutokueleweka katika jamii ambapo sasa ameondoka kwenye utegemezi.

“mafanikio yanaonekana kwasababu kabla kila kitu nilimtegemea baba yangu lakini sasa namudu kuendesha maisha yangu” alisema Saida

Ali Said Juma ni msimamizi wa mkuu  kwa wakulima Kupitia  alisema wakulima waliowafikia ni wale wamekuwa na kasi ya uzalishaji sambamba na kuwa na uhakika wa masoko.

“tulichogundua ni kuwa wakulima wanaomiliki miundombinu ya maji au tuliowasaidia miundombinu ya maji ni wakulima ambao wana uwezo wa kuzalisha kwa uharaka na uzalishaji wao ni mkubwa na wana masoko ya uhakika”

Alisema msimamizi huyo

Mtaalamu wa kuendeleza sekta ya kilimo Dk Anasia Gasper Maleko yeye alisema ongezeko la  uzalishaji wa bidhaa za mbogamboga viungo na matunda  ni miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana katika mradi huo Jambo ambalo linapelekea wakulima wadogowadogo kunufaika katika sekta hiyo.

 

Alisema mradi huo umekuja kuongeza nguvu kwa wakulima wadogowadogo ili kuongeza mnyororo wa Thamani katika uzalishaji hivyo aliwataka wakulima hao kuzidi kufuata utaratibu wa wataalamu wa kilimo kwa maendeleo zaidi.

 

 

Mradi wa mboga mboga viungo na matunda unatekelezwa na chama Cha wandishi wa habari Wanawake TAMWA Zanzibar,Community Forest Pemba na PDF kuwa kushirikiana na jumuia za Ulaya ili kuweza kufanikisha malengo ya wakulima wadogo wadogo katika kuimarisha mnyororo wa Thamani katika kilimo chao

Post a Comment

0 Comments