Ticker

6/recent/ticker-posts

Watu wenye ulemavu kielelezo tosha cha uwajibikaji


 

Mkurugenzi wa Idara ya Watu wenye Ulemavu Zanzibar Bibi Abeda Rashid Abdulla

Na Ahmed Abdullah

Wakati Dunia ikiendelea kupigania haki za watu wenye ulemavu visiwani Zanzibar baadhi ya watu wanaendelea kuwa na mtazamo potofu unaoonesha kuwa watu wenye ulemavu hawawezui kufanya kazi kama watu wengine wasiokua na ulemavu.

Mtanzamo huu potofu unaendelea kuenziwa na kizazi hadi kizazi na kuufanya kuendelea na inaamini imekua ikiwaathiri kisaikolojia watu wenye ulemavu kwa namna moja au nyegine na kupelekea baadhi ya kukata tamaa kabisa na kubaki kuwa watu wanaosubiri kudra za Muungu.

Licha ya mtazamo huu potofu kwa baadhi ya watu lakini Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na wanaharakati imekua ikisimama imara kupingana na jambo hili kwa kutoa fursa sawa kwa watu wenye ulemavu na inapobidi hutazamwa wao zaidi hususan kwenye sekta ya ajira.

Katika siku za hivi karibuni mtendaji mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Hemed Suleiman alikiri mna kusema watu wenye ulemavu ni muhimu na wachapa kazi zaidi maofisini wanapopatiwa fursa

Alisema Watu Wenye Ulemavu wana nguvu na uwezo mkubwa wa kufanya kazi kama walivyo Watu wengine kwenye uwajibikaji, lakini kinachohitajika kwa Jamii inayowazunguuka ni kukubali kuwapa dhamana kwa mujibu wa Maarifa, Elimu na Vipaji walivyobarikiwa.

Hata hivyo Mh. Hemed alisema Watu hao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbali mbali ndani ya Jamii hasa lile la kudhalilishwa kijinsia na matokeo yake hubaguliwa na kudharauliwa mambo yanayokwenda kinyume na haki za Binaadamu.

 

Alisema wakati Serikali ikiendelea na wajibu wake katika kuzingatia utatuzi wa changamoto za Watu hao wenye Mahitaji Maalum, Wananchi pamoja na Taasisi za Kijamii lazima zifikie maamuzi ya kuondosha manyanyaso hayo kwa kuwapatia fursa wanazostahiki ili nao wajihisi kuwa sehemu ya Jamii.

Akizungumza na mwandishi wa Makala hii Akitoa Mkurugenzi wa Idara ya Watu wenye Ulemavu Zanzibar Bibi Abeda Rashid Abdulla alisema kuna mafanikio makubwa kwa kiasi hususani haki za watu wenye ulemavu,akitolea mfano miaka ya nyuma ilikua si jambo la kawaida kumkuta mtu mwenye ulemavu ameajiriwa ofisini.

Alisema hivi sasa kwa mujibu wa takwimu zao watu wenye ulemavu takribani kila wizara wapo na wanafanya vyema kuliko mtazamo potofu walionao baadhi ya watu.

‘’Kuendelea kufanya kwao vyema huku ni kielelzo tosha kuwa watu wenye ulemavu wanachapa kazi na ni watu wanaopaswa kuthaminiwa’’aliongezea.

Mwandishi pia amezungumza na mmoja kati ya mtu mwenye ulemavu              Juma Kheri alisema yeye binafsi haoni kama ulemavu wake ni sehemu ya kukos fursa bali ulimpa ari kuongeza bidii ili afanye vizuri tangu akiwa darasani.

Alisema bidiii hiyo ndio iliomfanya afaulu vizuri na kupata nafasi ya ajira yenye uhakika,pamoja na hayo aliwataka watu wenye ulemavu wote kuongeza bidiii na kuonesha uwezo wanapopata fursa.

Post a Comment

0 Comments