Ticker

6/recent/ticker-posts

Uhuru wa kujieleza kichocheo cha maendeleo ya Taifa

 


Na Ahmed Abdalla

Imelezwa kuwa Uhuru wa kujieleza ni jambo muhimu katika kila Taifa linalohitaji kupiga hatua zaidi katika sekta mbali mbali.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa TAMWA-ZNZ Dkt,Mzuri Issa wakati wa mkutano maalumu uliojikita kuipitia sheria ya habari visiwani hapa huku lengo kuu likiwa ni kutoa mapendekezo katika upatikanaji wa sharia mpya.

Alisema jamii ikiwa huru kutoa mawazo yao ndio njia muhimu ambayo watu hupata kuyasema yale ambayo wengine wanadhani hayapaswi kusemwa huku wakitumia fursa hiyo kukandamiza wengine au kuficha mabaya yao.

Wakati mkurugunzi huyo wa TAMWA-ZNZ akiyasema hayo mratib wa Baraza la Habari Tanzania (MCT)upande wa Zanzibar Shifaa Said Hassan alisema kuna haja kubwa sana watu kuwa huru kutoa maoni yao ingawa uhuru huo pia unapaswa kuheshimiwa na kutowakashifu wengine.

Alisema iwapo sheria bora ya habari itapatikana Zanzibar ana imani mengi zaidi ya kimaendeleo yanaweza kutokea ikiwemo watu  kuelimika zaidi kwa kujifunza kupitia wengine.

Sambamba na hayo aliitaka jamii kwa ujumla iwapo sheria mpya iatakayokuja itatoa uhuru wa kujieleza watu hawana budi kuutumia uhuru huo vyema na kuepuka kujingiza kwenye matatizo zaidi ya kisheria.

‘’Kupewa uhuru wa kujieleza hakumaanishi mtu ama watu watukane au kukashifu wengine badala yake wanapaswa kuutumia uhuru huo vizuri kwa maslahi ya Taifa.

Awali wakichangia katika mkutano huo miongoni mwa wadau katika sekta ya habari walisema wanatamani sana kuona sheria mpya ya habari inapatikana visiwani hapa kwani iliopo sasa haiendani na mazingira ya binadamu wa karne hii.

Miongoni mwa wadau hao ni mwandishi wa habari wa kujitegemea Tallib Ussi alisema Zanzibar kama Mataifa mengine ulimwenguni kwa sasa isingepaswa kutumia sharia ya habari yenye changamoto za hapa na pale.

Alisema sheria inayohitajika sasa ni hile ambayo haitaacha chembe ya hofu kwa wadau na wananchi kwa ujumla huku ikiviacha vyombo vya habari na wananchi kwa ujumla kutumia haki zao za kikatiba ikiwemo ya uhuru wa kujieleza pamoja na kupokea na kutoa habari.

Post a Comment

0 Comments