Ticker

6/recent/ticker-posts

Akimbia Baada Ya Kutuhumiwa Kulawiti

 


Jeshi la Polisi Mkoa Wa Kusini Unguja bado linaendelea kumsaka ndugu. Khamis Abdalla Abdalla mkaazi wa Ndijani Mseweni aliyekimbia baada ya kutuhumiwa kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka tisa ambaye anasoma darasa la tatu jina limehifadhiwa.

 

Tukio hilo lilibainika Julai 30 mwaka huu nchana kweupe huko Ndijani Mseweni wilaya ya kati huku ikidaiwa kuwa mtuhumiwa huyo ameshafanya matukio kama hayo kipindi cha nyuma.

 

Baba mzazi wa mtoto huyo aliema mara baada ya kugundua kuwa mtoto wake huyo katendewa itendo hicho moja kwa moja alimfikisha hospitali kwa ajili ya vipimo na akagundulika kuwa ni kweli ameshafanyiwa kitendo hicho kiovu.

 

“kaonekana kwa macho ndani ya nyumba mimi nilipoletewa mtoto skumkosha nikaenda nae hospitali mnazi mmoja baada ya vipimo Daktari akaniambia mwanangu kaingiliwa kinyume na maumbile” alisema baba wa mtoto huyo

 

Alisema machungu wanayopita wazazi wanaopatwa na majanga hayo ya kudhsaaslilishiwa watoto wao ni makubwa hivyo huku akiviomba vyombo vya sheria kuchukuwa hatua stahiki kwa watu wanaotenda matendo hayo.

 

“mimi mwenyewe tokea jana sijaweza kula chakula chohote wa sijapata usingizi kutokana na kitendo alichofanyiwa mwanangu/’ Aliongezea baba huyo

 

Massoud Said Abdalla ni sheha wa shehia ya Ndijani mseweni alisema jambo hilo halitaki kuvumiliwa huku akisema kuwa ameshawapanga askari jamii wa shehia hiyo kuendelea kumtafuta mtuhumiwa huyo ili kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.

 

“baada ya upata taarifa hii nimeshawaelekeza askari jamii ili kumkamata na kumpadisha mahakamani” alisema sheha huyo

 

Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa kusini unguja kamishna msaidizi wa polisi Suleiman Hassan Suleiman amesema walipata taarifa ya yukio hilo la ulawiti ambapo walimsaka mtuhumiwa huyo ila alikimbia mara tu baada ya kutenda kosahilo.

 

“mtuhumiwa alikimbia na juhudi za kumtafuta zinaebdelea ili kumfikisha katika vyombo vya sheria” alosema kamanda huyo

 

Post a Comment

0 Comments