Ticker

6/recent/ticker-posts

Kifungu Kinavyowapa Mawaziri Nguvu Kuliko Mahakama

 


Na Berema Suleiman:

Sheria ya Wakala wa Habari, Vitabu na Magazeti namba 5 ya mwaka 1988, iliyofanyiwa marekebisho kwa Sheria Na. 8 ya mwaka 1997, ni moja kati ya sheria zinazotumika kuendesha shughuli za vyombo vya habari Zanzibar.

Moja wapo ya vifungu vyake vinavyokosolewa kwa kiasi kikubwa na wadau wa habari ni Kifungu cha 30(1), ambacho kinampa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya habari kusimamisha chapisho au gazeti lolote kwa madai ya maslahi ya umma au usalama wa taifa.

Vifungu hivi vimeibua mjadala mpana miongoni mwa wanaharakati wa haki za binadamu, waandishi wa habari pamoja na  wanasheria kwa kutaka kufaanyiwa marekebisho ya sheria mpya yaa habari kwa maslahi ya tasnia ya habari na taifa kwa ujumla.

Kifungu hiki kinaeleza kuwa:
“Waziri anaweza,  kusimamisha kwa muda au kuzuia kwa ujumla uchapishaji au usambazaji wa gazeti a ikiwa ataona kuwa maudhui yake yanaweza kuhatarisha usalama wa taifa, amani ya umma, au maadili ya jamii.”

Hii ina maana kuwa Waziri wa Habari anaweza, bila kuhitaji kibali cha mahakama, kutoa amri ya kusitisha gazeti kutokana na tathmini yake binafsi juu ya yaliyomo kwenye chapisho hilo.

Makala hii ilizungumza na wanasheria ambae pia ni wakili waa kujitegemea  Thabit Abdalla alisema kuwa kifungu hiki kinaipa serikali mamlaka makubwa mno yanayoweza kutumika vibaya dhidi ya uhuru wa vyombo vya habari.

“Sheria hii ni ya zamani na inakiuka misingi ya utawala bora na uwajibikaji. Waziri anakuwa na mamlaka ya mwisho, bila nafasi ya gazeti au mmiliki wake kujitetea. Hili linakiuka haki ya kusikilizwa na misingi ya haki za binadamu,” alisema Thabit.

Alieleza kuwa, katika nchi zinazoheshimu demokrasia, maamuzi ya kusimamisha gazeti hufanywa na mahakama kupitia mchakato wa wazi wa haki.

Aidha alisema ni wajibu wa mamlaka husika kuwa mstari wa mbele katikaa kuhakiisha sheria mpya ya habari inafanyiwa marekebisho ili wandishi wa habri na vyombo vya habari kufanya kazi kwa weledi katika kutoa tarifa zinazowajibisha viongozi.

Kwa upaade wake mjumbe wa kamati ya kitaalaamu ya masuala ya sheria za habari Zanzibar (ZAMECO)  Abdalla Mfaume alisema na kukiri kwamba kutokana na kifungu hicho kinaathiri uhuru wa habari na vyombo vya haari kuyokanana mamlak makubwa aliyopewa waziri kaatika kufungia vyombo vya habari ikiwemo magazeti hivyo alisemaa kuna haja ya kuwa na uwiano kati ya uhuru wa habari na maslahi ya taifa.

“Ni kweli tunahitaji mabadiliko ya sheria hii ili kulinda uhuru wa vyombo vya habari, lakini hatuwezi pia kupuuza athari hasi za maudhui yanayoweza kuleta chuki au uchochezi,” anaeleza Mfaume.

Hata hivyo, anashauri kuwe na tume huru ya habari itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza na kutoa maamuzi badala ya waziri mmoja pekee.

Pamoja na hayo kwa upande wake muandishi wa habari mkongwe Jabir Idrisa, ambaye amewahi kukumbwa na adhabu ya kufungiwa kwa gazeti alilokuwa analiandikia  alisema iwapo sheria haitafanyiwa marekebisho kwa vigungu vinavyokwaza uhuru wa habari basi maendeleo hayawezi kuongezeka.

“Sheria hii imekuwa chombo cha kuua uhuru wa kujieleza. Waandishi wanaandika kwa woga, wakihofia gazeti kufungiwa. Hii si afya kwa demokrasia,” alisema Jabir.

Anasisitiza kuwa Zanzibar inahitaji sheria mpya ya habari itakayoendana na katiba, mkataba wa kimataifa wa haki za binadamu, na maendeleo ya teknolojia.

Kwa upande wake mtetezi wa haki za binadamu THRDC Shadida  Omar kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) alisema sheria hiyo ni kandamizi na inakinzana na mikataba ya kimataifa ambayo Tanzania (ikiwemo Zanzibar) imeridhia, kama vile Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCPR).

“Sheria hii inatoa mianya ya kudhibiti vyombo vya habari visivyoegemea upande wa serikali. Tunapaza sauti kudai mabadiliko ya haraka ya sheria hii,” alisema Shadida.

Pia  alipendekeza  kusema kuwa kila mmoja ana haki ya kufanya kazi bila ya woga na hofu katika kutekeleza majukumu yake hivyo ni wajibu wa taasisi husika kuhakikisha sheria mpya ya habari inapatikana kwa maslahi mapana ya wandishi wa Habari na vyombo vya habari hapa nchini.

Kwa miaka mingi, Kifungu cha 30(1) cha Sheria ya Magazeti na Vitabu kimekuwa chanzo cha mgongano kati ya serikali na vyombo vya habari.

Wadau mbalimbali na wandishi wa habari wana mtazamo wa pamoja kuwa, ili kujenga jamii yenye uhuru wa kujieleza na kupata taarifa, kuna haja ya kuifanyia marekebisho sheria hii kwa kuzingatia katiba ya Zanzibar, haki za binadamu, na muktadha wa sasa wa kidemokrasia.

 

Post a Comment

0 Comments