Ticker

6/recent/ticker-posts

Kutokuwepo Kwa Sheria Rafiki Kunawakwaza Waandishi Wa Habari



 Na Siti Ali, Zanzibar:

FANI ya habari ni kama fani nyengine inaongozwa kwa sheria na kanuni mbalimbali hivyo waandishi wanapaswa kuzifahamu sheria na kanuni hizo sambamba na kuzitambua vyema zile sheria na ibara zote zinazokwaza uhuru wa vyombo vya habari ili waweze kutekeleza majukumu yao zaidi.

Lakini waandishi wa habari zanzibar bado wanaumiza kichwa kuhusu marekebisho ya sheria na hata kuamua kuwa nakauli mbiu “uhuru wa vyombo vya habari na mageuzi ya sera na sheria za habari zanzibar” katika siku ya waandishi wa habari duniani 2024.

Kwa muda mrefu (1988) licha ya wadau mbalimbali kutoa na kuwasilisha mapendekezo ya kutaka  mapungufu yaliyopo kwenye baadhi ya sheria za habari yafanyiwe marekebisho, lakini utekelezaji wake bado umekuwa wa kusuasua jambo linalopelekea mazingira magumu ya utendaji kazi wa waandishi wa habari nchini.

Kwa bahati mbaya kilio cha waandishi wa habari  Zanzibar hakijapata muombezi hadi sasa, hii inatokana na misukosuko wanayokumbana nao kila siku wakiwa katika majukumu yao ya kila siku.

Wakati wa maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari  duniani mwaka 2024, Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania,  (TAMWA Znz), Dkt. Mzuri Issa alielezea kwamba mchakato wa mabadiliko ya sheria za habari umekuepo kwa miaka mingi lakini bado sheria hizo ambazo nyingi ni za muda mrefu zimekwama kurekebishwa.

"Sisi wengine tangu tuko waandishi chipukizi tunazungumzia kupata  sheria mpya za habari, tangu 2008 kwa kweli ni muda mrefu, tunahitaji kusimamia jambo hili kwa umoja wetu  hatimae tupate sheria mpya za habari Zanzibar,

“Licha ya kuwasilisha ripoti ya mapendekezo yao kwa mamlaka husika ikiwemo kukutana na Rais wa Zanzibar pamoja na waziri anayeshughulikia masuala ya habari,lakini bado jitihada zetu zinagonga mwamba kwasababu kila mara tunachopewa ni ahadi tu kwamba sheria ziko mbioni kurekebishwa , " alieleza dkt. Mzuri .

Kikwazo kikubwa sheria iliyopo haifanani na wakati  uliopo kutokana na ukuaji wa sayansi na teknolojia kwani hivi sasa dunia umetoka kwenye   mfumo wa analogi na kuhamia digitali hivyo kutoa nafasi ya mambo kufanyika kwa haraka na ufanisi,

Hivyo hata utendaji kazi na mazingira ya uwendeshaji wa vyombo vya habari umebadilika na kusababisha sheria zinazosimamia vyombo hivi pia kupaswa kubadilika.

 

 Mwandishi wa Zanzibar  anasimamiwa na sheria zisizopunguwa sita ,lakini nyingi zao ni za kudhibiti  na si  kumlinda ili aweze kufanya kazi zake vizuri .

 Miongoni mwa sheria zinazompatia mwandishi wa habari maelekezo namna gani afanye na kutoa Adhabu kwa mfano ukiangaliya sheria inayoitwa ya Usalama wa Taifa na. 8 Mwaka 2010, Sheria ya Takwimu, na. 9 ya Mwaka 2015 ,Sheria ya Uchaguzi,na.4 mwaka 2018, na sheria ya Tume ya  Utangazaji na. 7 ya Mwaka 1997 iliyofanyiwa marekebisho na Sheria na.1 ya Mwaka 2010, zote zipo kwa kumpa fursa ya kufanya kazi lakini hazina nafasi ya kumlinda na kumuendeleza mwandishi wa habari.

“sheria inayotoa nafasi kwa Waziri au Taasisi ni Sheria ya Usajili wa wakala wa habari,magazeti na vitabu, ya na.5 ya mwaka 1988 kama ilivyorekebishwa na sheria na. 8 ya mwaka 1997 ambapo inamtaka  waziri kulifungia gazeti  kwa manufaa ya umma au kwa maslahi ya taifa.kufanya hivyo ni kuingilia kati mwenendo wa utoaji wa taarifa, utangazaji, uandishi au kufungia na kusitisha chombo cha habari kisifanye kazi, hali hiyo ikiendelea kuachwa uhuru wa habari kitanzini ”, amesema Mwinyimvua Abdi Nzuki, katibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar  (ZPC).

Mwandishi wa habari Mkongwe Salim Said Salim alieleza uwepo wa sheria bora ni muhimu katika kuwezesha mazingira bora ya waandishi wa habari kuwajibika.

"Vyombo vya habari ni washirika wa maendeleo, hivyo kuwa na sera na sheria bora itawawezesha waandishi wa habari kuwa na mazingira rafiki katika kutekeleza majukumu yao," alifahamisha, mwandishi wa habari huyo mkongwe Zanzibbar.

“Nidhahiri kwamba hakuna sheria rafiki kwa sisi waandishi wa habari kwani hata wakati wa ufanyaji wa kazi hivyo hutufanya kutokutumiya maadili wakati wa baadhi ya utekelezaji wa baadhi ya majukumu yetu ya kuihabarisha jamii na kukosekana kwa usawa wa mafanikio kati yake na wateja wake na kupelekea ukandamizaji wa sheria na kupata madhara makubwa yanayoweza kuathiri usalama wake” Jesse Mikofu mwandishi kutoka kampuni ya mwananchi ameelezea.

Jabir Idrisa Mwandishi wa Habari Mkongwe amekiri kwa kusema kuwa ‘’kutokana na kuwa sheria za habari zilizopo si rafiki kwa waandishi wa habari hivyo hukabiliwa na changamoto nyingi  zinazowakwaza kutekeleza  majukumu yao.

Miongoni mwa changamoto hizo ni mwandishi kufungiwa asiandike kwa muda , kuporwa vifaa vyakevya kazi , kunyimwa uhuru wa kusambaza na kuchukua  habari, pamoja na kutishiwa amani”anaeleza Jesse

  “Sheria rafiki za habari zinasaidia  waandishi wa habari kufanya kazi zao bila ya hofu wakiamini kwamba sheria zilizopo zinawalinda .lakini kinyume chake ,kukosekana kwa sheria rafiki ,inasababisha hofu kwa waandishi na vombo vya habari,kunadumaza demokrasia na utawala bora .

“Nchi ambayo haina sheria rafiki za habari inaweza kuchelewa kupata maendeleo kwa sababu changamoto zinazowakabili wananchi haziwezi kuibuliwa na kufika haraka kwa mamlaka husika” ameeleza Juma Khamis Juma (Mwanasheria)

Bishifaa Said Hassan Mjumbe wa Kamati ya Wataalamu wa Habari Zanzibar (ZAMECO) tutashirikiana na waandishi wa habari kuongeza kasi ya uchechemuzi na utetezi juu ya sheria hizi kandamizi kwa vyombo vya habari na waandishi wa habari kwa ujumla.

Na  tunaamini kuwa sauti na kalamu zao zinafika mbali sana kwa haraka zaidi, hivyo basi ni wajibu  kuhakikisha munatumiya kalamu  vizuri katika kuhakikisha munaandika habari na makala mbalimbali juu ya sheria hizi kusudi zifanyiwe maboresho.

Licha ya kufanyiwa mrekebisho kwa mfano Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari za Magazeti na Vitabu na. 5 ya Mwaka 1988 iliyofanyiwa marekebisho na kubana zaidi na Sheria na. 8 ya mwaka 1997 Sheria hizi bado vipo vifungu visivyotoa uhuru wa kutoa taarifa na kujieleza na kutoa nafasi ya kuuficha ukweli wa jambo kwa kulinda maslahi ya umma au kwa kulinda amani na utulivu .

Hivyo basi ni vyema serekali na mamlaka husika kulifanyia kazi suala la sheria za habari ili kuepusha usumbufu unaotokea kwa vyombo vya habari na waandishi kwa ujumla.


Post a Comment

0 Comments