Ticker

6/recent/ticker-posts

Athari Zinazopatikana Kwa Waandishi Wa Habari Wanaponyimwa Uhuru Wa Taarifa



Na Siti Ali, Zanzibar:

MWANDISHI wa habari ni mtu ambaye ana jukumu la kutafuta, kukusanya, kuandika na kusambaza habari kwa wasomaji, wasikilizaji na watazamaji katika jamii. Ili kuifanya vyema kazi yake kwa kuzingatia ukweli, kuepuka kuchukua taarifa feki,kuzingatia  usahihi, kutoegemea upande wowote, kuzingatia muda, kufanya usawa katika vyanzo vyake na kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Kutokana na majukumu hayo humfanya mwandishi wa habari kuwa mfano bora na kuwafanya wengine kuwajibika katika ufanyaji wao wa majukumu ya kila siku. Hii ni pale ambapo kalamu yake inapofanya kazi ya kukosoa  kukemea au kushauri hali inayopelekea serikali kuchukua hatua juu ya jambo lililozungumzwa na mwandishi wa habari.

Licha ya kuuona umuhimu wa mwandishi wa habari katika jamii lakini pia wapo baadhi ya watu ambao si waadilifu ambao wanawanyima uhuru waandishi kupata taarifa hali ambayo inarudisha nyuma juhudi zao pamoja na kumnyima mwanajamii  haki yake ya kupata taarifa .

Tunaelewa kwamba siku zote muungwana ni yule anayemtafuta mmiliki wa kitu anachokitaka kwa lengo la kupatiwa ridhaa au baraka na hapa nimewatafuta baadhi ya waandishi wa habari ambao wamekutana na changamoto hiyo na kusema kuwa.

“Waandishi wa habari visiwani Zanzibar wanakabiliwa na changamoto kadhaa katika utekelezaji wa majukumu yao ikiwamo kupata vitisho kutoka kwa viongozi wa serikali, ukiandika chochote kinachohusiana na taasisi au mamlaka fulanikama haikuwafurahisha kuyaondosha hewani au kuyakana, hali hii ni ukandamizaji wa haki ya kupata kupata kusambaza habari “amesema Thuwaiba Habibu mwandishi wa habari wa kujitolea.

“Changamoto nyingi wanazokumbana nazo waandishi wa habari zinatokana na  sheria tulizo nazo kwa mfano sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari ,Magazeti na Vitabu na.5 ya Mwaka  1988 iliyofanyiwa marekebisho na sheria na.8 ya mwaka 1997 na Sheria ya Tume ya Utangazaji ya Mwaka 1997 pamoja na marekebisho yake Mwaka 2010 .kutokana na vikwazo vilivyomo ndani ya sheria hizo ,waandishi wa habari wanapata hofu kutoa baadhi ya taarifa .” Amesema Thuwaba Habibu .

Wanahabari wengi visiwani Zanzibar hukosa kutekeleza jukumu la kupata taarifa na hapa ile kauli ya mjomba nsaidie ndiyo hudhibitika kwa kuwa vyombo binafsi hukosa fursa sawa na vyombo vya serikali. Kama alivyoeleza mdau wa habari kutoka visiwani humo, ambapo ndiyo kulikoanza waandishi wa habari wanawake

“Wanahabari hatuna uhuru katika ufanyaji wa kazi ya kutafuta taarifa hususani vyombo binafsi ambavyo hukandamizwa na baadhi ya watumishi wa umma kupitiya nyadhifa walizo nazo” alisema Bakari Haji Khamis mwandishi wa habari wa kujitolea.

Naye Mauwa Juma Salim mwandishi wa habari wa TIFU TV anaelezea changamoto wanazokumbana nazo ikiwamo baadhi ya waandishi wa  habari kunyimwa fursa ya kuchukua taarifa muhimu ili kuihabarisha jamii kwa kisingizio cha chombo cha binafsi na badala yake kupewa fursa mwandishi wa chombo cha serekali hii inamaana ya kwamba uhuru wa habari haupo kwa waandishi wa habari kutoka vyombo binafsi hivyo kupelekea wananchi wanaopendelea kusikiliza au kusoma taarifa zinazoandikwa /kutangazwa na vyombo hivyo , kukosa haki ya kupata taarifa.

“Vile vile wanahabari hatuna uhuru katika ufanyaji wa kazi ya kutafuta taarifa hususani vyombo binafsi ambavyo kukandamizwa na baadhi ya watumishi wa umma kupitiya nyadhifa walizo nazo”ameeleza Mauwa.

 Mkurugenzi  wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA ZNZ) Dk. Mzuri Issa anasema kama wanahabari wanakosa haki ya kupata taarifa na jamii haiwezi kupata taarifa zinazowahusu, hivyo inapaswa utekelezaji wa haki  ya kupata habari na kujieleza kama ilivyo ndani ya  Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, (ibara ya 18).na ile iliyomo katika katiba ya zanzibar kifungu na. 18(1) na (2)

Ibara na.18 (1) kinasema Bila ya kuathiri sheria nyengine za nchi kila mtu anayo haki ya uhuru wa maoni,kujieleza,kutafuta kupokea na kusambaza habari na mawazo yake kupitia chombo chochote cha habari bila ya kujali mipaka ya nchi na pia anayo haki na uhuru wa kutokuingiliwa mawasiliano yake .

Kutokana na ukongwe wa sheria zilizopo ambazo zinaweka wajibu wa waandishi wa habari kutafuta taarifa lakini   hakuna wajibu wa waajiri wa serikali kutoa taarifa hizo, inakuwa ni vigumu kwa wanahabari kufanya majukumu yao ya kuuhabarisha umma habari zisizoegemea upande na habari zenye ukweli usio na chembe ya shaka .

Fatma Ramadhan Juma pamoja na  Juma Mohd wakaazi wa Mfenesini wanasema kuwa wanachangamoto kazaa ambazo wangependa zijulikane kwa jamii na hata kwa wenye mamlaka lakini wanashindwa kuzielezea  kwani wamekuwa wakitoa taarifa kwa waandishi lakini hazijapata nafasi ya kutolewa kwenye vyombo vya habari.

Fatma anasema kuwa hali hiyo inaonesha kuwa kuna mchujo mkubwa katika vyombo vya habari na taarifa zinazowagusa wananchi moja kwa moja mara nyingi huwa hazipewi nafasikwa sababu ya woga au kuna watu wanalinda tonge zao.

“Kila siku tunatoa taarifa kwa waandishi wa habari lakini tukifuatiliya taarifa tulizotoa hazijatumwa au zikitumwa baadhi ya maneno yanatolewa ambayo ndiyo malengo yetu tuliyokusudia kwa serikali na hufanya hivyo kwaajili ya usalama wao”anaeleza bwana Juma.

Kupitia makala hii leo naomba kuwauliza swali hivi jamii ikikosa taarifa je, kuna mtu anaweza kuishi kwa amani katika dunia hii? Wakati unafikiriya hilo, napenda kuwakumbusha maneno ya wahenga yasemayo usimdharau akubebaye na usiangalie ulipoangukia, angaliya ulipotelezea watumishi wa umma sasa wanabudi la kufikiriya njia nzuri ya kutatua tatizo hili ili jamii kupata taarifa kwa wakati sahihi kupitiya vyombo vya habari.

Post a Comment

0 Comments