Ticker

6/recent/ticker-posts

Uchumi Mdogo Kikwanzo Kwa Wanawake Kufikia Uongozi

 


Na Amrat Kombo, Zanzibar

Dunia ni darasa la kujifunza mengi, mazuri na yenye machungu na mengine humuacha mtu anajiuliza masuali ambayo jawabu yake haipati na kila akiona anaikaribia hopotea kama moshi hewani.

Uzoefu umetuonyesha kwamba kukosa na kupata ni majaaliwa, lakini badhi ya watu hujiengea dhana na kuiamini  hata kufikiria yupo mtu au kikundi cha watu ndio kikwazo cha kwake yeye kupata maendeleo.

Hapo zamani wazee  wetu  walishikana mikono, wakasafishiana nyoyo zao na kusaidiana kwa hali na mali, iwe wakati furaha au wa shida. Lakini sasa mambo yamebadilika, nguvu ya pesa imechachamaa.

Kila mtu masikini anapojaribu kujipapatua anakuta anapanda mlima ambao kilele chake hakioni. Yote haya yametokana na  wengi wenye mamlaka na madaraka kutojali shida za mtu masikini .

Katika kutaka kujuwa juhudi za wanawake kutaka kushika nafasi za uongozi ili wasaidie wanawake wezao watokane na umasikini nilikwenda Kikungwi, mkoa wa Kusini Uguja.

Huko nilikutana na mwanamama  mcheshi, mkarimu, jasiri na mchapa kazi, mwenye rangi ya jongoo na sura nzuri ya duara na umbile lenye haiba ya mwanamke aliyenieleza mengi juu ya safari yake ya kugombea uongozi.

Bahati Issa Suleimani, mwenye umri wa miaka 51 , mwenye watoto 6 alithubutu kuwania nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo ya katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika mwaka 1995,  na Mwenyekiti wa  Umoja Wanawake Tanzania  mnamo mwaka 2017.

“Katika mwaka 2020 niligombea nafasi ya udiwani, lakini  kwa bahati mbaya sikufanikiwa, sikukata tama. hivyo  niligombea tena nafasi ya Mwenyekiti Wanawake Tanzania (UWT) wa jimbo mwaka 2023 ila sikufanikiwa’’,alielezea.

Kukosa huko hakukumkatisha tama  Bahati kwa kuamini iposiku atafanikiwa.

Amesema ilimsikitisha kuwa sasabu ya kutofanikiwa ni kuona kilichothaminiwa katika hizo chaguzi ni pesa na sio utu na uwezo wa mtu.

‘’ Umaskini wangu ndio uliopelekea nikose nafasi kwani baadhi yawananchi waliona siwezi kuleta maendeleo kwakuwa sina  pesa ,hivyo wakaona bora wasinipigie  kura.”ameongezea

 Alichobaini ni kuwa jamii iliyomzunguka  ina mtazamo hasi juu ya wanawake kushiriki katika siasa na jambo la kushangaza ni kuona wanawake wenzake waliokuwa mstari wa mbele kumkandamiza.

 “Ukiangalia nafasi ya udiwani wagombea tulikuwa 6 wanaume watano na mwanamke nilikuwa peke yangu na kwa nafasi ya ubunge wagombea wote watatu walikuwa wanaume. .”Amesema

Bahati ameniambia anaona ni vyema vyama vya siasa vikachukua juhudi za kuwainua wanawake kiuchumi ili hatimaye wawe na nguvu ya kugombea uongozi.

Safari  haikuishia kwa  Bahati tu niliendelea kusonga mbele hadi Kombeni na kukutana  na Aisha Haji Mzee  aliethubutu kuwania nafasi ya uwakilishi katika Jimbo la Mwanakwerekwe.

" Katika mwaka 2020 nilithubutu kugombea uwakilishi katika Jimbo  la Mwanakwerekwe lakini sikufanikiwa kupata aliongea  kwa masikitiko huku akitikisa kichwa." 

 Alisema kukosa fedha ndio kikwazo kilichopelekea kushindwa kwake, kwani hakua na uwezo wa kupiga kampeni ,kuandaa mikutano na kuwafikia watu kwa wakati. ingawa chama kilimsaidia  lakini kilishiwa njiani kutokana na hali duni ya chama hicho. amesema

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chamacha Adatadea  Ali Makame Issa, amesema  ukosefu wa Ruzuku kwa baadhi ya vyama vya siasa ni sababu kubwa ya kushindwa  kusaidia wanawake kushika nafasi za uongozi.

“Ili chama kiweze kumsaidia wanawake kuingia kwenye nafasi ya uongozi kinatakiwa kiwe na Ruzuku ambayo itakayoweza  kutatua changamoto wanayokabiliana nayo.”Amesema

Katibu Mkuu wa Chama cha Makini, Ameir Hassan Ameir, amesema   bado chama chao  ni kichanga na hakina vyanzo vya mapato ambavyo vingeweza kupunguza tatizo hilo, alipendekeza serikali itowe ruzuku maalum kwa wagombea wanawake  ili kuwasaidia kutimiza malengo.

Ushauri huo umenifanya nitembelee ofisi ya msemaji wa serikali  Hamza Hassan Juma ambae ni waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar  na kueleza kuwa serikali inatoa ruzuku kwa kufuata sheria.

" Kifungu cha 16 cha sheria ya vyama vya siasa hairuhusu kila chama kupewa ruzuku isipokuwa chama ambacho kina uwakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi, au chama ambacho kimepatakura nyingi." Amesema

Hata hivyo, amesema ruzuku sio  sababu ya kuwazuia vyama vya siasa kusaidia wanawake kuingia katika uongozi kwa sababu vyama vya siasa vinatakiwa kutoa michango katika matawi yao ili kusaidia shughuli za kisiasa.

“Serikali haitoi ruzuku kwa vyama visivyotimiza vigezo vya kupewa Ruzuku kama vile kuwa na wanachama wachache wa kuweza kuwaweka viongozi wao katika chombo cha kutunga sheria ”Amesema

Hata hivyo, zipo taasisi zinazohamsisha wanawake kujikomboa kiuchumi kwa lengo la kuwasaidia katika harakati  za kisiasa .Katika Idara ya Maendelao ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto niliongeana na mkurugezi wa idara hiyo, Siti  Abasi Ali, Amesema

Wamehamasisha vikundi mbalimbali vya wajasiriamali wanawake kuchukuwa mikopo isiyo na riba ya viko 19 ambayo itawasaidia kuimarika kiuchumi na kuwajengea uwezo katika shughuli zao za kisiasa.

“Tumepata vikundi vya wajasiriamali wanawake 1,971 vikiwa na wanawake 59,753 lengo ni kuhamasisha wanawake waweze kufanya biashara ili kuhakikisha wanapata fedha ambayo itawainua kiuchumi katika kugombea nafasi za uongozi.

Amewashauri  wanawake kuchangamkia fursa za mikopo iliyopo ili kuwasaidia katika shughuli zao za kimaendeleo na kisiasa.

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake  Tamwa – Zanzibar kinatoa mafunzo ya uongozi kwa wanawake na kutatua changamoto zinazowakabili.

Mkurugenzi wa Chama hicho  Dkt.Mzuri Issa alikiri kwa masikitiko kwamba wanawake wengi wamekumbana na changamto walipotaka kugombea uongozi.

“Tumetoa mafunzo ya uongozi kwa wanawake kwa  kushirikiana na Jumuiya ya wanasheria wanawake Zafela na zidi ya wanawake 100 tumewapatia mafunzo hayo Unguja na Pemba. Tulichogungundua ni asilimia 50 ya wanawake wamekutana na changamoto ya uchumi.”Amesema

Ukiangalia wawakilishi wa majimbo 50 Zanzibar wanawake 8 sawa na asilimia 16,wabunge wa jamuhuri ya muungano kutoka Zanzibar kwenye majimbo 50 wanawake wanne ,sawa na asilimia 8  mawaziri 6 sawa na asilimia 33,makatibu wakuu 7 sawa na asilimia 39.

Kwa upande wa  wakuu wa mikoa mwanamke mmoja  sawa na asilimia 20,wakuu wa wilaya wanne sawa  na asilimia 36 na masheha wanawake 79 sawa na asilimia 20, wanaume 309 sawa na asilimia 80 kwa masheha wote wa Unguja na Pemba ambao ni 388.

 

Post a Comment

0 Comments