Ticker

6/recent/ticker-posts

Wanavikundi Wachekelea Ujio Wa Mradi Wa Kijaluba

Baadhi ya bidhaa zinazotengezwa na kikundi cha kuweka na kukopa cha Mwanzo Mgumu kilichopo Michamvi Kae

Na Ahmed Abdulla, Zanzibar:

INAELEZWA kuwa ujio wa mradi wa kijaluba kumewasaidia wananchi wengi walionufaika na mradi huo kuinua hali zao za kiuchumi pamoja na kupata elimu ya utengenezaji wa bidhaa mbalimbali.

Mradi huo uliolenga ushirikishwaji wa kwatu wenye ulemavu katika kukuimarisha hali za jamii uliakisi matakwa ya kuzingatia usawa katika kutekeleza majukumu ya kujitafutia riziki za halali.

Wapo ambao kwasasa wanaweza kufanya kazi za mikono ikiwa ni pamoja na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo sabuni,mafuta ya kujipaka pamoja na mapambo.

Hii ni kutokana na mafunzo mbalimbali waliopatia lengo kuu ni kuondoa utegemezi eti kwa kisingizio kuwa ni mwenye ulemavu.

Ramadhan Haji Vua ni Mwenyekiti wa kikundi cha kuweka na kukopa Tutambuane kilichopo shehia ya Kikadini, Jambiani alisema moja ya eneo lililowasaidia kwa kiasi kikubwa ni eneo la mfuko wa jamii.

“Tulipata maafa ya mvua kubwa, nyumba zikaingia maji hivyo waliopata huo msiba wakafarijika na mfuko huu wa jamii ndio nikaona huu mradi umetutoka  gizani” alisema

Kwa upande wa bi Asha Amour kutoka kikundi cha Nyota Ya Bahati chenye jumla ya wanachama 30 kilichopo Bwejuu Kusini Mwa Kisiwa Cha Unguja alisemema ujio wa mradi huo umewafanya wakwamuke kwenye janga la umasikini kwani baadhi yao wameanzisha biashara zilizotokana na kukopa fedha katik vikundi vyao.

“Kuhusu kusomesha na matibabu hayanipigi chenga hii ni kutokana na faida ninayoipata kwenye kikundi” alisema Bi Asha

Jee baada ya mkupuo wa kwanza wa ukusanyaji wa hisa za vibubu vya Vikundi vinavyonufaika na mradi wa Kijaluba kuna hamasa iliyoongezeka kwenye Vikundi hivyo?

Mohammed Haji Khamisi ni katibu wa kikundi cha Tutambuane alisema kutokana na faida iliyopatikana kwenye mkupuo wa kwanza kumetoa hamasa kwa wananchi kujiunga na kikundi chao hali iliyoifanya idadi kuongezeka kutoka wanachama 25 hadi 30.

“Tunaendeleza kwa sababu tumeona mafanikio yake jinsi gani tunavyojisaidia na ndio mana wanachama wameongezeka” Alisema

Kwa upande wa kikundi cha mwanzo mgumu kupitia kwa mshika fedha wao Mwanahamis Shaes Khamis Alisema ni faraja kwao kuja kwa mradi wa kijaluba kwani umewarahisishia kupata mikopo kwa wakati na isiyokuwa na riba.

“Kila tulipoomba mikopo kwa ajili ya kuanzisha biashara zetu tulikwama kwa sababu ya riba ila kuja kwa kijaluba sasa tunakopa,tunafanya biashara na tunajiinua kiuchumi. Alisema

Kwa upande wake Afisa program kutoka chama cha waandishi wa Habari Wanzawake Tanzania upande wa Zanzibar (TAMWA-ZNZ) Khairat Haji alisema wanavikundi waliwapatia mafunzo mbalimbali ikiwemo ya kutambua haki zao (watu wenye ulemavu), elimu ya kuweka na kukopa, umuhimu wa kuweka akiba,jinsi ya kutumia mikopo na kufanya biashara, kutengeneza bidhaa pamoja na mafunzo ya uendeshaji wa biashara.

“tumeona wengine wafunguwa biashara ya sabuni sasa walipatiwa mafunzo ya jinsi ya kuendesha biashara ili ilete faida” alisema Khairat

Aidha aliendelea kusema kuwa “tunashukuru lengo limefanikiwa kwasababu wakati tunaanza ilikuwa ngumu kutokana na mitazamo ya jamii kufikiria kuwa watu wenye ulemavu ni watu wa kupewa na sio mtu anateweza kuweka kitu”

Khairat pia alisema ni jambo la kufurahisha kuona wanajamii wanafurahia uwepo wa mradi huo na kuona tija ya vikundi vyao inapatikana.

Mradi wa kijaluba ni wa miaka miwili ulianza mwaka 2022 na unatarajiwa kukamilika Mwezi Oktoba mwaka huu na unatekelezwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania upande wa Zanzibar (TAMWA-ZNZ) na shirikisho La jumuiya za watu wenye Ulemavu Zanziba (SHIJUWAZA).

 

Post a Comment

0 Comments