Ticker

6/recent/ticker-posts

Juhudi Za Asasi Za Kiraia Zasaidia Kuweka Usawa Wa Kijinsia

 

DKt. Samia Suluhu Hassan Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Ahmed Abdulla:

Katika miaka ya karibu asasi nyingi za kiraia ziliopo Zanzibar zimeongeza nguvu katika kujenga mazingira ya kuwa na usawa wa kijinsia kwenye nafasi za uongozi.

Lengo ni kuona nafasi hizi zinashikiliwa bila ya vikwazo wa aina yoyote ule wa kijinsia ili kuimarisha mfumo wa utawala wa demokrasia.

Nguvu hizi zitakuwa na tija kama patakuwepo matokeo yatakayoleta mabadiliko kwenye jamii.

Katika harakati hizi zipo jumuiya ambazo  unaweza kusema zimekuwa mstari wa mbele kwenye kutoa elimu juu ya suala hili na kuwa mstari wa mbeke katika utetezi wa wanawake, kuanzia akiwa mtoto hadi mtu mzima.

Miongoni mwao ni Chama Cha waandishi wa Habari Wanawake TAMWA-Zanzibar ambayo imekuwa ikifanya juhudi za kuhakikisha wanawake wanapata nafasi za viongozi, kama ilivyo kwa wanaume.

Mkurugenzi wa TAMWA-Zanzbar, Dk. Mzuri Issa, akiiambia Zanlight blog kuwa kumalizikwa hivi karibuni kwa mradi wa kuwawezesha wanawake kwenye kushika nafasi za uongozi isiwe sababu ya kuzuia harakati hizo ziendelee.

Badala yake iwe hatua ya kwanza ya safari ya kuhakikisha wanawake wanapata haki yao ya kushiriki katika kuiongoza jamii na nchi kwa ujumla.

“Sasa ni wakati wa kuendeleza kampeni kwa kutoa habari  zinazohusu wanawake ili kuleta uchechemuzi wa kufikia lengo kuu la kuwa na usawa  wa kijinsia kwenye nafasi za uongozi”, alieleza

Alisema mradi wa viungo unaoendeshwa na jumuiya yake na ule wa kijaluba pia unasaidia unachochea nguvu ya mwanamke, hasa katika eneo la kiuchumi.

Aliwataka wale walionufaika na miradi hiyo  ifikapo mwaka  2025 wajitahidi kuleta matokeo chanya kwenye uchaguzi mkuu.

Jukwaa la Walimu Wanawake wa Kiafrika (FAWE) upande wa Zanzibar nalo ni shirika linalojipambanua kwa kuwawezesha wanawake kiuchumi na kielimu.

Mpango wake wa kuwawezesha wanawake kwenye uongozi umelenga zaidi katika elimu na uchumi ikiwa kwa kuwapatia wanawake mafunzo na mitaji ya kuendesha shughuli mbali mbali.

 

Mkurugenzi wa Shirika hilo kwa  Zanzibar, Winnifred Yatuwa Mamawi, alisema lengo ni kuhakikisha mwanamke anasimama mwenyewe kusaka nafasi za uonguzi.

“Tumewaingiza watetezi wa masuala ya jinsia wanawake na wanaume kwa sababu wanaume ndio wamekuwa kikwazo kikubwa cha wanawake kusoga mbele kupata nafasi za uongozi”, alisema

Miongoni mwa hatua ziliochukuliwa na FAWE ni kutoa mitaji ya Shilingi millioni tatu na sasa kiwango kimeongezwa na kuwa milioni 10.

Lengo ni kuendelea na mradi huo na mtaji kufikia zaidi ya milioni 20 ifikapo mwaka 2025.

“Tunatarajia ifikapo mwaka 2025 wanawake wawe wanaweza kuendesha biashara zao wenyewe na wengine kujisimamia katika  kusaka uongozi”, aliongeza

Taasis nyengine inayofanya kazi hii ni Community Forest Pemba inayojikita katika kumuwezesha mwanamke kwa njia tatu zinazolenga kumuimarisha  kiuchumi.

Hii itamuwezesha kukweka  malengo yake pasina kuwepo kwa changamoto ziliopo hivi sasa.

Mkurugenzi wa jumuiya hiyo, Mbarouk Mussa Omar, aliieleza Blog kuwa katika mradi wao wa kuwawezesha wanawake kukabiliana na hali za kiuchumi wamelenga kuwfikia wanawake 400 katika kuwaandaa  kuwa viongozi.

“Kwa ujumla tumelenga kuwafikia wanawake 4,000, katika hao tunakitaji wanawake 1,800 tuwapeleke kwenye uhifadhi wa misitu, 1,200 kwenye mikoko, 600  kwenye masuala ya Jinsia na wengine 400 watakwenda kwenye masuala ya uongozi.

Matarajio ya nguvu hizi

Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekuwa akiwataka wanawake kujitokeza kwa wingi  kugombea  uongozi, sambamba na walioteuliwa  waonyeshe uwezo na uadilifu mkubwa.

Ni dhahiri kuwa inawezekana kwa Zanzibar kufikia mgao wa nafasi za uongozi kati ya wanaume na wanawake kufikia  asilimia 50 kwa 50.

Lakini hili linahitaji kufanyiwa kazi na zaidi na wanawake, kwanza kwa kujiamini na kujitokeza kuwania nafasi za uongozi.

Vile vile upo muhimu wa kuwabadilisha mitazamo wanaume wanaodhani  mwanamke hawezi kuongoza.

 

Post a Comment

0 Comments