Ticker

6/recent/ticker-posts

TAMWA Yapania Kuwanowa Wanawake Viongozi

 


Na Ahmed Abdulla, Zanzibar:

Mkurugunzi wa Chama cha Waandishi wa habari wanawake Dk Mzuri Issa amewataka wanawake nchini kujiamini na kuondokana na woga wakati wa kugombea nafasi za Uongozi kwa lengo la kuleta mabadiliko katika jamii.

Dk Mzuri ameyasema hayo wakati wa mkutano uliowashirikisha wasomi wanawake kutoka vyuo vikuu tofauti wakipata mafunzo juu ya kugombea nafasi za Uongozi uliofanyika katika Ofisi za  TAMWA ZNZ , Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema kwa sasa dunia imetambuwa umuhimu wa mwanamke na imeamini mwanamke ni Kiongozi kutokana na utofauti uliopo kati yake na mwanamme kwa kuwa na uwezo wa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja huku akitekeleza majukumu yake ipasavyo.

“Mwanamke anaweza kuwa mama, mke, mfanyakazi na Kiongoz na wakati huo huo akitekeleza  majukumu yote hayo kwa wakati mmoja  na akafanya vizuri katika kila sekta bila kuathiri upande wowote kama wengine wanavyodhani, Dk Mzuri Issa ,  Mkurugenzi TAMWA ZNZ.

Akitowa mafunzo hayo kwa wanawake wasomi Mshauri Elekezi Inilda Lulu Orio amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwasaidia kuwajengea uwezo wa kujitambuwa na nakutambuwa nafasi zao ili kufikia ndoto zao katika harakati za Uongozi.

“Nafasi ya wanawake kwa sasa inazidi kuongezeka kwa sababu kuna ukuwaji wa Elimu kwa jamii na hata watoto wakike wenyewe kwa sababu Uongozi unajengwa , tumeona baadhi ya jamii inavyowajenga watoto wa kike kuweza kujitambuwa na Ongezeko kubwa la Viongozi wanawake, Inilda Lulu Orio, Mshauri Elekezi.

Nae Mratibu wa mradi wa kuwawezesha wanawake kugombea nafasi za Uongozi (SWIL) Maryam Ame Chuom amesema kwa mda mrefu imeonekana wanawake wameachwa nyuma katika ngazi za maamuzi hivyo kwa sasa wanawake watumie fursa na haki yao ya kikatiba ya kuchaguwa na kuchaguliwa.

Aidha washiriki wa mafunzo hayo wamesema wamefarajika kupata mafunzo hayo na watakuwa mabalozi wazuri kwa wanawake na kupambana kugombania nafasi za ngazi za juu ili kuondosha mfumo dume uliotawala katika jamii.

“Matarajio yangu baada ya mafunzo haya ni kuwa Kiongozi mwenye kujiamini, mimi ni kiongozi , na baadaa ya hapo nitapambana kuwa kiongozi wa nagazi ya juu zaidi katika chuo change, Hudhaimat Haji Juma, Mwanafunzi wa Shahada ya Pili ya Uhasibu katika Chuo Kikuu cha Taifa, Campus ya Chwaka.

Mradi wa kuwajengea uwezo wanawake kugombea nafasi za Uongozi unaotekelezwa kwa pamoja na TAMWA ZNZ, PEGAO NA ZAFELA umewashirikisha wanawake kumi na tano kutoka vyuo Vikuu chini ya ufadhili ya NORWAY.    

 

 

 

Post a Comment

0 Comments