Ticker

6/recent/ticker-posts

Pondeza Afikia Walengwa Nusu Sadaka Ya Ramadhani

Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Ussi Salum Pondeza akimkabidhi mmoja wa wananchi wa Jimbo hilo mfuko wenye vyakula mbalimbali pamoja na bahasha yenye fedha taslim

Jumla ya watu 854 wa jimbo la Chumbuni wamefikiwa sadaka ya vyakula inayotolewa na mbunge wa jimbo hilo Ussi Salum Pondeza kwa mfungo huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Idadi hiyo ni sawa na asilimia 51.14 ya walengwa wote 1670 watakaofikiwa katika kipindi kizima cha mfungo huo.

Akizungumza mara baada ya zoezi la kugawa sadaka kwa kaya maskini za shehia sita za Jimbo la Chumbuni, mbunge wa jimbo hilo Ussi Salum Pondeza alisema azma yake ni kuona wananchi wake wanakuwa na uhakika wa futari katika mfungo huo.

“nimejiwekea kila mwezi mtukufu wa Ramadhani niwe natoa sadaka kwenye jimbo langu nan je ya jimbo langu” alisema Pondeza

Alisema kwa leo amewafikia watu wenye hali duni ya kiuchumi ili awapatie sadaka hiyo hali itakayowawezesha kumufu futari ndani ya siku kadhaa.

“Tumewatafuta ambao hawako vizuri kiuchumi ili tuwapatie sadaka hiyo iwasaidie kwa siku chache. Aliongezea Mbunge huyo

Kwa upande wa wananchi waliopatiwa sadaka hiyo walimpongeza mbunge huyo kwa kuwajali na kuwathamini katika kipindi hiki cha mfungo huku wakiwaomba viongozi wengine kufuata nyayo za mbunge huyo.

“mbunge anatusaidia sada kwa mfano leo ingekuwa sina futari hii ingetusaidia” alisema mmoja wa wananchi

Mbali na zoezi hilo mbunge huyo pia aliwapatia sadaka ya fedha watoto wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo La Chumbuni Ussi Salum Pondeza akimkabidhi Mtoto wa jimbo hilo sadaka ya Fedha Taslim


Post a Comment

0 Comments