Ticker

6/recent/ticker-posts

Wenye ulemavu wanahitaji msaada wa kisaikolojia




Na Ahmed Abdullah


Kwa sasa siajabu tena ukifika mjini Unguja majira ya mchana na jioni kukutana na watu wenye ulemavu wanaofanya kazi ya kuomba watu pesa na kuna wakati wameanza kuwa kero na mara kadhaa wamewahi kurudishwa wanapoishi.

Makala ya uchunguzi imebaini kuwa uwepo wa watu hao ambao kikawaida huletwa na gari maalumu kila ifikapo asubuhi na kugawiwa maeneo maalumu ya kuwekwa kwa mchana kutwa huku wakiendelea na kazi hiyo.

Mila na desturi za kizanzibar hazikuwahi kushuhudia tabia hiyo ambayo kwa kiasia kikubwa inachafua taaswira ya watu wenye ulemavu kiujumla.

Inaaminika kuwa kuna watu maalumu walioamua kuwageuza watu wenye ulemavu kama sehemu ya mtaji kwenye maisha yao na ndio maana inasemakana huwakodia hadi nyumba na kuwaweka pamoja.

Kwa mujibu wa sheria namba 9 ya mwaka 2006 Wajibu wa kulinda haki za watu wenye ulemavu (20)Watu wenye ulemavu hawatabaguliwa na kudhalilishwa kwa namna yoyote ile na katika ngazi yoyote na katika ngazi zozote zile kutokana na sababu ya ulemavu.

Swali ambalo tunaweza kujiuliza ni kwanini watu wenye ulemavu hukubali kuwa mtaji wa biashara hii?

Kwa uchunguzi wa ndani kabisa unabaini baadhi ya watu wenye ulemavu wamekua wakiathirika kisaikolojia kwa kukosa kwao watu muhimu kwenye mfumo mzima wa maisha yao ambao wangewasemesha na kuwajenga kinadharia ili waweze kufanya shughuli mbali mbali za kujingizia kipato.

Kukosa kwao nadharia hii muhimu ya stadi za maisha imekua ikiwakosesha uwezo wa kufikiri watu hawa na kuamini kuwa wao si sehemu ya jamii wanayoweza kufanya lolote lile bali wanastahiki kuomba na kupatiwa fedha kitu ambacho kubadilikwa inawezekana.

Katibu mtendaji wa Baraza la watu wenye ulemavu Zanzibar Ussi Khamis anasema kuna tatizo la baadhi ya watu wenye ulemavu kukosa ukaribu na watu muhimu kwenye maisha yao.

Alisema watu wenye ulemavu huzaliwa wakiwa pungufu hivyo hujiona si sehemu wanayo stahiki kufanya lolote lile bali wanahitahi msaada tu,na kwamba mtazamo huo unahitaji kubadilishwa.

Alisema tabia ya omba omba inaanzia tokea wakiwa na umri mdogo kwa sababu ya kukosa misingi ya utaftaji na ndio maana huwa warahisi wanaposhawishiwa na watu wenye nia ovu.

Kwa masharti ya kutotajwa jina mmoja ambae alikua mkaazi wa karibu na nyumba waliopangiwa au waliopanga wenye mjini Unguja alisema ilikua kawaida kila siku ifikapo saa 12 za asubuhi kuiona gari maalumu iliokua inakuja na kuwachukua kwenye nyumba hio watu hao na badae huwarejesha jioni.

Alisema utaratibu huo ulimfanya yeye kushangazwa na kutaka kujua haswa ni nani wanaofanya alichokiita na kudhani biashara na ndipo walipo taarifu uongozi wa shehia na hatua zilianza kuchukuliwa.

Wasemavyo wahusika.

Kwa mazingira magumu mmoja ya watu wenye ulemavu alikuabali kuzungumza na mwandishi wa habari hii bila ya kujua kuwa ni mwandishi na kumuelewa kuwa wanaweza kukusanya hadi elfu hamsini baadhi ya siku na inaweza kwenda hivyo hadi wiki nzima.

Alisema kuna watu ambao wanawapelekea pesa hizo na badae hufanyika mgao na wahusika ukizingatia wana mahitaji ambayo hupatiwa kila leo hivyo wanalazimika kuwa sehemu ya wanaochangia huduma hizo.

Msimamo wa Serikali.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa mara kadhaa imewahi kuzungumzia jambo hilo nma kuonesha kukerwa kwake na kusema haipo tayari kuona watu wenye ulemavu kuheuka kuwa omba omba.

Kauli ya TAMWA-ZNZ

Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA-ZNZ Dkt,Mzuri Issa alisema ulemavu usiwe sababu ya wahusika kutofanya kazi bali wanapaswa kujitambua kuwa ni sehemu ya maumbile ambayo wamejaaliwa.

Pamoja na hayo aliwataka waandishi wa habari kujikita zaidi kuandika habari zinazohusu watu wenye ulemavu na harakati zao huku lengo kubwa likiwa ni kuwasaidia kwa hali na mali.

Post a Comment

0 Comments