Ticker

6/recent/ticker-posts

Dkt Mzuri awakumbusha wanahabari Haki ya Kujieleza


 


Na Ahmed Abdalla

Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa habari TAMWA-ZNZ Dkt Mzuri Issa amesema vyombo vya habari vinawajibu wa kujiwekea utaratibu na kuandaa vipindi maalumu ambavyo vitaangazia haki ya uhuru wa kujieleza.

Aliyasema hayo wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari katika mafunzo maalumu ambayo yanalenga kuwakumbusha wanahabari visiwani Zanzibar jinsia ya kuthamini haki hiyo muhimu.

Alisema tafaiti zinaonesha kwa miaka mingi visiwani Zanzibar wanahabari wameisahau haki hio ya kujieleza na kuwaacha wananchi wengi wakishindwa kupaza sauti zao.

Alisema iwapo vyombo vya habari vitarudi na kujikita katika kutengeza vipindi na kuandaa habari zinazohusu haki ya kujieleza vinaweza kuibua mengi ambayo yataweza kulisaidia Taifa kwa ujumla.

Sambamba na hayo Mkurugenzi huyo alisema iwapo uhuru wa kujieleza utatumia vyema unaweza pia kuwakuza waandishi wa habari na kuvipa sifa zaidi vyombo vyao wanavyofanyika kazi.

Kwa nyakati tofauti baadhi ya washiri wa mkutano huo uliowezeskwa kwa mashirikiano na Internews Tanzania walisema kwa muda mrefu wameisahau haki hiyo ya kujieleza.

Walisema kwa kusahau huko wanadhani wamekosa kuwatendea haki wananchi wengi kila leo na ndio maana sasa wameamua kuanza upya na kukusanya habari nyingi zitakazo husu haki ya kujieleza.

Miongoni mwa wanahabari hao ni Khatib Slemain alisema mara baadha ya kupata mafunzo hayo atajikita na uandishi wa Makala zitakazowagusa zaidi watu na sauti zao.

 

Post a Comment

0 Comments