Ticker

6/recent/ticker-posts

Dkt,Mzuri Ataka Mabadiliko Sheria Ya Habari Zanzibar

 


Na Ahmed Abdulla

 

Mkurugenzi wa TAMWA-ZNZ Dkt, Mzuri Issa amesema kwa miaka mingi Zanzibar imekua ikitumia sheria ya habari ilioanza kufanya kazi tangu mwaka  1987 hadi sasa sheria ambayo imekua na chanagamoto nyingi kiutekelezaji.

Dkt, Mzuri aliyasema hayo wakati alipokua akizungumza na wadau na wawakilishi wa vyombo mbalimbali vya habari visiwani hapa katika mkutano malumu ulioandaliwa na TAMWA-ZNZ kwa kushirikiana na Intenews Tanzania.

Alisema Zanzibar kama sehemu ya Jamuhuri ya Muungano yenye sheria yake ya habari inapaswa kupiga hatua ikiwemo kufanyia mabadiliko ya sheria hio.

Alisema katika dunia hii ya utandawazi na uhitaji wa taarifa hadi sasa Zanzibar imekua ikinyima uhuru wa habari kwa baadhi ya vipengele kwa mfano sheria imeweka wazi kuwa jeshi la polisi linaweza kuzuia chapisho lolote lile iwapo watahisi kuna hali ambayo wao haitawaridhisha.

Alisema jeshi la polisi na taasisi nyengine hazipaswi kupewa uhuru wa kisheria kuminya uhuru wa kutoa na kupata habari.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Hits Radio Hafidh Kassim alisema kumekua na vikwazo vingi katika tasnia ya habari.

Alisema hadi sasa redio nyingi Zanzibar zimekua zikifanya kazi kwa maelekezo aliyoadaia yanatoka juu kwa baaadhi ya vipindi.

Alisema kuna wakati ukifika vyombo vya habari hupelekewa hadi barua ya onyo wanapofanya vipindi vya mahojiano na baadhi ya watu.

Nae katibu mtendaji wa Klabu ya waandishi wa habari Pemba (PPC)Ali Mbarouk alisema mabadiliko ya sheria ya habari ni kitu ambacho hakipaswi kuepukika kwa sasa.

Alisema sheria iliopo imepitwa na wakati na kwamba kila inapochelewa kubadilishwa ni sawa na kuendelea kuwakandamiza walio wengi.


Post a Comment

0 Comments