Ticker

6/recent/ticker-posts

-Dkt. Mzuri Akutana Na Ugeni Wa Mataifa 14 Kujadili Vita Dhidi Ya Udhalilishaji


 Na Ahmed Abdulla

Mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania kwa upande wa Zanzibar  TAMWA-ZNZ Dkt, Mzuri Issa amepokea ugeni wa watu 14 kutoka Mataifa tofauti ulimwenguni, ugeni ambao ulifika ofisi za Tunguu Wilaya kati Unguja.

Ugeni huo uliokua na lengo la kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya TAMWA-ZNZ inavyofanya kazi kwa mafanikio makubwa katika jamii.

Akizungumza na ugeni huo Dkt,Mzuri alisema ni sehemu ya kujifunza na kubadilishana uzoefu ukizingatia miongoni wa wageni hao wanafanya kazi katika mashirika tofauti yanayofanana katika utendaji wao wa kazi za kila siku.

Alisema ni muhimu sana kubadilishana uzoefu juu ya mbinu za kupambana na udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto.

Pia alisema kuna changamoto katika mapambano ikiwemo mila na desturi kwa baadhi ya wanafamilia kuendelea kuyaficha matendo ya udhalilishaji wakihofia aibu.

Awali kiongozi wa msafara huo Anna-Keira alipongeza juhudi kubwa inayofanywa na na chama hicho katika mapambano ya udhalilishaji.

Akaendelea kusisitiza zaidi na kusema ni muhimu juhudi hizo kuendelezwa kwa sababu zinalenga kuwalinda wanawake na watoto kwa lengo la kuhakikisha jamii inabaki salama.

Post a Comment

0 Comments