Ticker

6/recent/ticker-posts

ZASWA FC Waupiga Mwingi Dhidi Ya ZRB

Timu ya waandishi wa habari za michezo Zanzibar

 

 

Timu ya waandishi wa habari za michezo Zanzibar inayonolewa wa kaimu kocha mkuu Suleiman Nyanga jana Agosti 16, 2021 ilifanikiwa kuitandika mabao 3-2 timu ya bodi ya mapato Zanzibar ZRB katika mchezo uliochezwa majira ya saa 1:00 usikukatika uwanja wa Mao Tse Tung.

Magoli ya ZASWA FC yalifungwa na Is-haqa Mant,Kheir Abdulkadir na Aboubakar Kharith P ambapo mabao yote hayo yalifungwa kipindi cha kwanza huku mabao ya Timu ya ZRB yakifungwa na Lukman Kassim.

Mara baada ya ushindi huo kaimu kocha mkuu wa ZASWA FC Suleiman Nyanga aliesema kikosi cha ZRB hakikuwa na ubora mkubwa wa kuwafunga hasa katika kipindi cha kwanza hivyo kuwafanya kuongoza mabao hayo matatu katika kipindi cha kwanza kizima.

“Hakika kikosi hakikuwa kizuri sana katika mchezo wa jana ndio mana tulipata kuongoza bao 3-0 katika kipindi cha kwanxza” alisema kocha huyo

Kocha huyo aliendelea kusema kuwa pia timu yake ilifanya udhaifu katika kipindi cha pili hali iliyowarehusu ZRB  kurejesha mabao mawili na ubao wa matokeo ukasomeka 3-2.

“Kwa udaifu wa kikosi changu ulioufanya kipindi cha pili kwa bahati mbaya tumerejeshewa mabao mawili na kuyafanya matokeo kuwa 3-2” aliongezea kocha huyo

Alisema udhaifu wa kikosi chake umetokana na kutocheza mechi kwa muda mrefu huku akisema ni takriban mwezi mmoja sasa timu haifanyi mazoezi ambapo amesema ushindi huo umetokana na ari ya wachezaji,uzowefu wake na benchi zima la ufundi pamoja na sapoti ya mashabiki.

Sambamba na hayo alisema anauongozi wa ZASWA FC uandae utaratibu wa mazoezi ili watengeneze timu iliyo bora kwa ajili ya ushindani zaidi.

Tokea timu ya ZAZWA ianze kunolewa na kocha Nyanga imecheza michezo mitano ambapo imeshinda michezo mitatu na kupoteza michezo miwili.

 


Post a Comment

0 Comments