Ticker

6/recent/ticker-posts

DKT. MWINYI AMTENGUA KATIBU WAKE.

 

RAISI wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi ametengua uteuzi wa katibu wa Raisi Bwana. Suleiman Ahmed Saleh kuanzia leo Disemba 14.

Raisi Dkt. Mwinyi amefanya utenguzi huo kwa uwezo aliopewa chini ya kifungu namba 53 cha katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na kifungu namba 12(3) cha sheria ya utumishi wa umma namba 2 ya mwaka 2011.

Katka taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na kutiwa saini na katibu wa baraza la mapinduzi ambaye pia ni katibu mkuu kiongozi Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee imesema kuwa Bwana. Suleiman atapangiwa kazi nyengine.

Ikumbukwe mnamo Novemba 4 Dkt. Mwinyi alimteua bwana. Suleiman Ahmed Saleh kuwa katibu wa Raisi wa Zanzibar.



Post a Comment

0 Comments